Thu, 14 Jan 2021
Chanzo: habarileo.co.tz
Rais wa Malawi Lazarus Chakwera, ametangaza siku tatu za kuomboleza nchi nzima kufuatia vifo vya mawaziri wake wawili, Lingson Belekanyama na Muhammad Sidik waliofariki jana kwa Corona.
Vifo vya mawaziri hao vilithibitishwa na Waziri wa Habari nchini humo, Gospel Kazako.
Lingson alikuwa Waziri wa Serikali za Mitaa huku Muhammad akiwa Waziri wa Uchukuzi.
Chanzo: habarileo.co.tz