Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mawakili wa Kenya waandamana kupinga vitisho vya Rais Ruto dhidi ya majaji

Majaji Kenya Mawakili wa Kenya waandamana kupinga vitisho vya Rais Ruto dhidi ya majaji

Fri, 12 Jan 2024 Chanzo: Bbc

Makumi ya mawakili wanaandamana katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, kujibu vitisho vya kukaidi amri ya mahakama yvilivyotolewa na Rais William Ruto.

Mawakili hao wanaandamana kutoka Mahakama ya Juu hadi afisi ya rais katika maandamano yaliyopangwa na Chama cha Wanasheria nchini (LSK).

Rais Ruto alikosolewa wiki iliyopita baada ya kutishia kutotii maagizo ya mahakama, akidai kuwa baadhi ya majaji ambao hawakutaja waliungana na wanasiasa wa upinzani kuzuia miradi ya utawala wake.

"Rais wa nchi hii hayuko juu ya sheria. Kwa hivyo, hatutarajii azungumze kana kwamba kutii amri za mahakama ni upendeleo anaofanyia nchi. Ni hitaji la kikatiba," rais wa LSK Eric Theuri alisema.katika mkutano na wanahabari siku ya Alhamisi.

Bw Theuri aliongeza kuwa LSK itafikiria kuanzisha mchakato wa kumuondoa madarakani Rais Ruto kwa "kukiuka katiba" ikiwa ataendelea na mashambulizi yake dhidi ya mahakama.

LSK imekusanya timu ya wanasheria kuwasilisha ombi katika Mahakama ya Juu dhdi ya Bw Ruto kwa kukiuka katiba, Bw Theuri aliambia gazeti la Standard.

Mawakili kadhaa maarufu nchini Kenya wamejiunga na maandamano hayo, akiwemo Makamu wa Rais wa zamani Kalonzo Musyoka na waziri wa zamani Eugene Wamalwa, ambao kwa sasa ni wanasiasa wa upinzani.

Jaji Mkuu Martha Koome na kinara wa upinzani Raila Odinga wiki jana walimuonya Bw Ruto kwamba kukaidi mahakama kutaanzisha hali ya machafuko nchini.

Chanzo: Bbc