Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Matunda ya handisheki: Raila atua Kisumu kwa ndege ya kijeshi

32544e2e89ad8097 Matunda ya handisheki: Raila atua Kisumu kwa ndege ya kijeshi

Sat, 29 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Rais Uhuru aliagiza Raila kupeperushwa hadi Kisumu kwa ndege ya kijeshi muda mchache baada ya kikao katika Ikulu

- Rais aliwaambia viongzoi wa Nyanza kuwa urafiki wake na Raila utakuwa na manufaa makubwa kwa eneo lao

- Rais na Raila watazindua miradi kadhaa ya maendeleo kabla ya sherehe ya Madaraka Dei Jumanne Juni 1

Kinara wa ODM Raila Odinga Ijumaa Mei 28 alipepea hadi Kisumu kutoka Nairobi kwa ndege ya kijeshi.

Raila, maarufu kisiasa kama Baba, alitua katika uwanja wa ndege wa Kisumu na kupokelewa na Gavana wa Kisumu Profesa Anyang Nyong.

Raila alisafiri Kisumu baada ya kufanya kikao na Rais Uhuru Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi ambapo aliwapeleka wandani wake kukutana na kiongozi huyo wa taifa.

Baada ya viongzoi hao kupokea ujumbe wa Rais, Baba alipewa ndege hiyo ya kijeshi ili kufika Kisumu ambapo atakuwa akipanga mambo kwenye 'ground' kabla ya Rais kufika Jumapili Mei 30.

Kulingana na afisa mmoja mkuu serikalini, ni rais pekee mwenye mamlaka ya kuruhusu ndege hiyo 'kuwabeba watu wengine'.

Raila na Uhuru wamekuwa na urafiki mkubwa tangu waingie kwenye mkataba wa handisheki ambapo wamekuwa wakipanga uongozi wa nchi pamoja.

Wakati wa kikao hicho cha Ikulu Ijumaa, Uhuru aliwaambia viongozi wa Nyanza kuwa lengo lao ni kuwacha historia ya kipekee wakiondoka.

Mimi na ndugu yangu (Raila Odinga) tunataka kuacha urithi ambapo vijana watakuwa na kazi, watakuwa na uwezo wa kupata mahitaji ya kimsingi na nchi ambayo raia wote wanajivunia kuwa Wakenya," Uhuru alisema katika mkutano huo.

Alidokeza kuwa kwa muda mrefu, siasa za chuki zimerudisha nyuma maendeleo ya taifa na vile vile kuzua changamoto ambazo alisema zinaweza kutatuliwa na viongozi wakiungana kwa ajili ya manufaa ya mwananchi.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke