Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Matiang'i asema ndoa baina ya maafisa wa polisi zitapigwa marufuku kikosini

29507b21f628f7ab Matiang'i asema ndoa baina ya maafisa wa polisi zitapigwa marufuku kikosini

Fri, 30 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Matiang'i ameuliza Wizara yake kutunga sheria zinazopiga marufuku maafisa wa polisi kuwa na uhusiano kimapenzi kazini

- Matiang'i alielezea kuwa agizo hilo litaundwa ili kuzuia visa vya dhuluma na utovu wa nidhamu ambavyo vimeongezeka katika idaya ya polisi

- Matamshi yake yanajiri karibu wiki tatu baada ya mlinzi katika afisi yake kumuua mkewe na kisha kujitia kitanzi

Waziri wa Usalama ya Ndani Fred Matiang'i ametangaza kuwa Wizara hiyo itaunda sheria mpya zinazopiga marufuku maafisa wa polisi kuwa na uhusiano wa mapenzi kazi

Akiongea wakati wa hafla ya ufunguzi wa kozi ya wakaguzi wa cadet katika Chuo cha Kitaifa cha Polisi cha Kiganjo, Nyeri, Matiang'i alielezea kuwa agizo hilo litatengenezwa ili kuzuia visa vya dhuluma na utovu wa nidamu ambavyo vimeongezeka katika idaya ya polisi.

"Maafisa wakuu watapigwa marufuku dhidi ya kuwa na uhusiano wa mapenzi na wadogo wao. Mmoja atalazimika kuacha huduma," alisema Ijumaa, Aprili 30.

Matamshi ya Matiang'i yanajiri karibu wiki tatu baada ya mlinzi katika afisi yake na mkewe, afisa wa trafiki, kuaga dunia kwa kile kilichoshukiwa kuwa mauaji na kujitia kitanzi.

Afisa wa Mkuu wa Kitengo cha Huduma Hudson Wakise alimpiga risasi na kumuua mkewe Pauline Wakasa kabla ya kujielekezea bunduki na kujitoa uhai.

Wakasa alipewa kutolewa kamili kwa sherehe lakini Wakise alizikwa bila polisi. Waliingiliwa katika nyumba zao tofauti za familia.

Wakasa alizikwa kulingana na utaratibu wa maafisa polisi naye Wakise alizikwa kama raia wa kawaida bila polisi. Kila mmoja wao alizikwa kwao.

Matiang'i aliwaomboleza wawili hao akisema kwamba alisikitishwa mno na yaliyotokea kuhusiana na wachumba hao.

"Ni suala ambalo linatisha ikizingatiwa kuwa maafisa wetu wachanga wanasumbuliwa kisaikolojia, na sasa tunapaswa kulizamia mzima mzima. Rambirambi zangu kwa familia ambazo zimeathirika na msiba huu," alidokeza.

Hata hivyo, wemngi mitandaoni walionekana kutofautiana vikali na semi za waziri huyo wakielezea shauku lao na jinsi amri hiyo itakavyotekelezwa.





Wiki iliyopita, kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga alielezea wasiwasi wake kuhusu visa vinavyozidi kushuhuiwa vya mizozo ya kinyumbani na watu kuuwana.

Kiongoozi huyo alielezea masikitiko yake kwamba watu wengi wanazidi kupoteza maisha yao kutokana na mizozo hiyo ambayo kilakuchao inalenga vichwa vya habari.

Raila, alitaka mazungumzo ya dharura ya kitaifa juu ya unyanyasaji wa kijinsia kufanywa kwa dharura ili kurejesha amani na kuwasaidia wanandoa kujua jinsi ya kutatua mizozo ya kinyumbani.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke