Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Matiang'i aongoza mkutano wa Raila na viongozi wa Kisii

C59fd1af4800ca95 Matiang'i aongoza mkutano wa Raila na viongozi wa Kisii

Fri, 2 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Matiang'i aliongoza kikao cha viongozi kutoka Gusii na Raila ambapo masuala mazito yalijadiliwaIlikuwa ni kikao cha kwanza kati ya Matiang'i na viongozi hao wanaoegemea ODM tangu walalamike alitumia mamlaka vibaya wakati wa uchaguzi mdogo wa BonchariRaila amekuwa na ushawishi mkubwa katika siasa za jamii ya Gusii ambapo ODM ni maarufuWaziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i ameibukia kuwa moja wa sauti nzito kwenye uongozi wa jamii ya Abagusii.

Alhamisi Julai 1, Matiang'i aliongoza kikosi cha viongozi wenzake kutoka jamii hiyo kukutana na kinara wa ODM Raila Odinga.

Raila alisema kikao hicho kilikuwa cha kujadili maendeleo ya eneo la Nyanza sawa na masuala mengine mazito ya kitaifa.

"Tumejadili masuala muhimu ya kitaifa na maendeleo ya eneo la Nyanza wakati wa kikao na viongozi kutoka jamii ya Gusii wakiongozwa na waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i na Gavana James Ongwae," alisema Raila.

Raila alikuwa ameandamana na mtoto wake wa kisiasa ambaye pia ni mwelekezi wa masuala ya kisiasa katika chama cha ODM Junet Mohamed.

Kikao hicho kilionekana kama mojawapo wa mbinu za Raila kuendelea kuwa na ushawishi katika jamii ya Gusii.

Aidha ni kikao kinachojiri baada ya viongozi wa Kisii wakiongozwa na Gavana Ongwae na Seneta Ong'era kumkashifu Matiang'i wakati wa uchaguzi mdogo wa eneo bunge la Bonchari.



Wakati huo viongozi hao walisema Matiang'i alikuwa akitumia polisi kumpigia debe mgombea wa Jubilee Zebedeo Opore.

Ni hali iliyotikisa urafiki wa handisheki huku chama cha ODM kikilalamika kuhangaishwa licha ya Raila kuwa rafiki wa serikali kupitia handisheki.

Mgombea wa ODM alishindi uchaguzi huo mdogo licha ya hayo na huenda viongozi hao walikubali kumaliza uhasama wao na Matiang'i.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke