Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maswali yaibuka kuhusu ziara ya DP Ruto kisiwani Zanzibar

C6c89c1abc18b2ff Maswali yaibuka kuhusu ziara ya DP Ruto kisiwani Zanzibar

Mon, 26 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Ruto alikuwa Kisiwani Zanzibar Jumamosi Julai 24 akiandamana na wandani wakeHaijabainika ajenda ya ziara hiyo lakini Makau Mutua akisema ilikuwa ya kujivinjariDP hakuchapisha ushahidi wa ziara hiyo kwenye kurasa zake lakini TUKO.co.ke ilipata picha yake akiwasili nchini humoNaibu Rais William Ruto Jumamosi Julai 24 alifanya ziara katika Kisiwa cha Zanzibari akiandamana na wandani wake.

Kambi ya DP Ruto imekuwa kimya kuhusiana na ziara hiyo ambayo ajenda yake bado haijabainika.

Upekuzi wa meza ya TUKO.co.ke umeonyesha hakuna ushahidi wa ziara hiyo katika kurasa za DP mitandoani.

Ruto hujulikana kwa kuchapisha picha za ziara yake au vikao na wandani katika mtandao wake wa Facebook na Twitter na kwa sasa si wazi ni kwa nini hakuna picha yoyote kuhusu ziara hiyo.



Ushahidi wa ziara hiyo uko katika picha ya pekee iliyopakiwa na mbunge wa bunge la Afrika Mashariki Simon Mbugua.

"Kigogo alipowasili Zanzibar," alisema Mbugua ambaye huwa ni mwandani wa kisiasa wa Ruto.



Read also

Uchunguzi wa Maiti kwa Mwili wa Konstebo Caroline Kangogo Wakosa Kufanyika

Hata hivyo, mbunge huyo hakutoa taarifa zaidi ya iwapo alikuwa ndiye mpokezi wa Ruto au ziara hiyo ilikuwa na lengo lipi.

Wakosoaji wa DP Makau Mutua na Junet Mohammed alizungumzia ziara hiyo huku wakifichua waliokuwa wameandamana na DP.

Walichapisha orodha ya walioandamana na Ruto Zanzibar na kutumia hilo kumtupia vijembe wakili tajika Ahmednassir Abdullahi.

"Wakili ahmednasir sioni jina lako hapa. Hii unajua ni ziara kubwa. Ni kama kigogo wako hawatambui Wasomali," Junet alimwandikia kwenye twitter.

Mchanganuzi Makau Mutua alisema ziara hiyo ilikuwa ya Ruto kutoa kijasho kwa kujivinjari baada ya kivumbi siasani.

Ahmednasir pia alimtupia mishale Makau akimkumbusha amekuwa akikutana na kinara wa ODM pia.

"Tofauti na wewe, mimi huomba tu katika misikiti. Na huwa sina haja ya kupiga picha nikiomba au baada ya kuomba. Lakini wewe najua penye huenda kuomba," alimwandikia Makau na kuchapisha picha yake akiwa na Baba.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690



Read also

Kitu Ilikuwa Safi: Tume ya IEBC Yasema Kuhusu Uchaguzi wa Kiambaa

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke