Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Masaibu ya DP Ruto: Chris Wamalwa asema huenda Naibu Rais akajiuzulu

F8c352181f084beb Masaibu ya DP Ruto: Chris Wamalwa asema huenda Naibu Rais akajiuzulu

Tue, 20 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- William Ruto ametengwa katika kuendesha shughuli za serikali tangu salamu maarufu ya Machi 2018 kati ya Rais Uhuru Kenyatta na aliyekuwa waziri mkuu Raila Odinga

- Alhamisi, Aprili 15, DP alikiri kwamba alidhalilishwa na serikali ya Jubilee, ambapo anahudumu akiwa afisa wa pili wa ngazi ya juu baada ya Uhuru

- Ruto, hata hivyo, alisema licha ya masaibu yake, hatajiuzulu wadhifa wake kwa sababu alichaguliwa na Wakenya

- Mbunge wa Kiminini Chris Wamalwa, hata hivyo, amesema huenda Ruto akajiuzulu kabla ya kutangaza rasmi kutnganaa na Uhuru

Mbunge wa Kiminini Chris Wamalwa amesema Naibu Rais William Ruto huenda akajiuzulu kabla ya Uchaguzi Mkuu ujao wa 2022.

Akizungumza na Citizen TV, mbunge huyo wa Ford Kenya alisema kuwa Ruto ambaye maisha yake katika chama tawala yamekumbwa na msukosuko ana wazia kujiuzulu na hatimaye kutangaza kutengana na bosi wake.

"Naibu rais huenda akajiuzulu lakini sio sasa. Atafanya hivyo kwa wakati unaofaa na utakaomwezesha kuwa na msuli wa kisiasa wa kuweza pia kupata huruma."

"Ninajua kuna watu wengi ambao wanajaribu kumsukuma nje .... lakini ikiwa atajiuzulu sasa, atakuwa hatarini sana ... sioni akikaa katika Jubilee hadi mwisho wa muhula; huenda akaacha miezi kadhaa kabla ya uchaguzi mkuu," Wamalwa alisema.

Naibu Rais ametengwa katika kuendesha shughuli za serikali tangu salamu maarufu ya Machi 2018 kati ya Rais Uhuru Kenyatta na aliyekuwa waziri mkuu Raila Odinga.

Amekuwa akikabiliwa na shinikizo la kumtaka ajiuzulu wadhifa wake, huku baadhi ya marafiki wa Uhuru wakimshutumu kwa kusema amekuwa akihujumu utawala wa Jubilee kutoka ndani.

Ruto kukiri kudhalilishwaMatamshi ya Wamalwa yalijiri siku chache baada ya Ruto kukiri amedhalilishwa na serikali ya Jubilee, ambapo anahudumu akiwa naibu wa Rais Uhuru.

Akizungumza Alhamisi, Aprili 15, Naibu Rais alithibitisha wazi kuwa sio kila kitu ndani ya chama tawala ni sawa na kwamba ametengwa.

Ruto alijutia kwa kile alichokiita malumbano mabaya, njama za kumuondoa madarakani, siasa za chuki vyote anavyoshuhudia kwa mara ya kwanza dhidi ya naibu rais nchini Kenya tangu uhuru mnamo 1963.

"Manaibu marais wengi wanapiganwa. Hiyo ni bahati mbaya. Nikipewa nafasi, sitakubali DP yangu kudhalilishwa jinsi DP za zamani zilivyodhalilika na vile vile nimedhalilishwa."

Ruto, hata hivyo, alisema licha ya masaibu yanayomwandama, hatojiuzulu kwa sababu alichaguliwa na Wakenya.

"Bado sijafika mahali ambapo ninataka kujiuzulu ... Watu wengine wanaamini wanaweza kunishinikiza nijiuzulu, lakini nataka kuwakumbusha kwamba nilichaguliwa. Sitawaruhusu washerehekee juhudi zao za kushinikiza mimi nje ya serikali," alisema.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke