Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Marekani yawataka raia wake kuondoka Ethiopia mara moja

35,000 Ethiopians Marekani yawataka raia wake kuondoka Ethiopia mara moja

Wed, 17 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imewaonya raia wa Marekani nchini Ethiopia kwamba haitaweza kuwahamisha iwapo hali ya usalama itazidi kuwa mbaya ghafla.

Afisa wa ngazi ya juu wa Marekani aliwataka raia wa Marekani kuondoka Ethiopia mara moja, akisema kuwa Washington haina mpango wa kuandaa uhamisho wa watu wengi, kama ilivyokuwa Afghanistan.

Marekani na Umoja wa Afrika zimekuwa zikiishinikiza serikali ya Ethiopia na waasi katika eneo la Tigray kumaliza mzozo wao, ambao umeua maelfu ya watu na wengine milioni mbili kuyahama makazi yao tangu ulipoanza mwaka mmoja uliopita.

Maafisa wa Marekani wanasema Marekani imesitisha kuidhinisha vikwazo dhidi ya pande zinazozozana, kwa sababu mazungumzo ya amani bado yanaendelea.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live