Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Marekani kuiondoa Uganda katika mkataba wa Agoa

Marekani Kuiondoa Uganda Katika Mkataba Wa Agoa Marekani kuiondoa Uganda katika mkataba wa Agoa

Tue, 31 Oct 2023 Chanzo: Bbc

Rais wa Marekani Joe Biden amefichua mipango ya kuzifukuza Uganda, Gabon, Niger na Jamhuri ya Afrika ya Kati kutoka kwa mpango maalum wa kibiashara wa Marekani na Afrika.

Nchi hizo ima zilihusika katika "ukiukaji mkubwa" wa haki za binadamu au kutopiga hatua kuelekea utawala wa kidemokrasia, rais alisema. Marekani ilianzisha Sheria ya Ukuaji na Fursa Afrika (Agoa) mwaka 2000.

Inazipa nchi zinazostahiki za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na ufikiaji bila ushuru wa Marekani kwa zaidi ya bidhaa 1,800.

Rais Biden alisema kuwa Niger na Gabon - zote mbili kwa sasa ziko chini ya utawala wa kijeshi kufuatia mapinduzi ya mwaka huu - hazistahiki Agoa kwa sababu "hazijaanzisha, au hazifanyi maendeleo endelevu katika kuanzisha ulinzi wa vyama vingi vya kisiasa na utawala wa sheria. ".

Pia alisema kuwa kuondolewa kwa CAR na Uganda kutoka kwa mpango huo kulitokana na "ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu zinazotambulika kimataifa" na serikali zao.

Mwezi Mei, serikali ya Marekani ilisema inafikiria kuiondoa Uganda kutoka Agoa na kuiwekea vikwazo nchi hiyo baada ya kupitisha sheria yenye utata dhidi ya mapenzi ya jinsia moja.

Chanzo: Bbc