Mon, 28 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watu 14 wamefariki dunia baada ya kutokea maporomoko ya ardhi katika mji wa Yaounde nchini Cameroon.
Kwa mujibu wa gavana wa eneo hilo, Naseri Paul Bea watu hao walikuwa wamehudhuria mazishi jana Jumapili Novemba 27, 2022 jioni.
Mamlaka zinasema kuwa vikosi vya uokoaji bado vilikuwa vinatafuta miili mingine na manusura.
Mashuhuda wamesema kuwa familia kadhaa za waombolezaji zilikuwa zimekusanyika chini ya hema kubwa wakati tukio hilo linatokea baada ya mvua kubwa kunyesha.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live