Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mapinduzi ya Niger: Rais aliyepunduliwa atembelewa na daktari wake

Mapinduzi Ya Niger: Rais Aliyepunduliwa Atembelewa Na Daktari Wake Mapinduzi ya Niger: Rais aliyepunduliwa atembelewa na daktari wake

Sun, 13 Aug 2023 Chanzo: Bbc

Rais wa Niger aliyepinduliwa Mohamed Bazoum ametembelewa na daktari ambaye pia alimletea chakula, mmoja wa maafisa wake ameliambia shirika la habari la AFP siku ya Jumamosi.

Hii inafuatia wasiwasi wa kimataifa juu ya afya na usalama wa rais na familia yake ambao waliripotiwa kuwekwa katika "hali ya kibinadamu".

"Ni sawa, kutokana na hali ilivyo," chanzo hicho kimeliambia shirika la habari la AFP.

Rais Bazoum, mwenye umri wa miaka 63, mkewe na mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 20 wamezuiliwa katika ikulu ya rais kwa zaidi ya wiki mbili tangu mapinduzi ya kijeshi yaliyoongozwa na Jenerali Abourahamane Tchiani yaliyoiangusha serikali yake.

Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Turk amesema hali ya kukamatwa kwa Bazoum "inaweza kuwa ni sawa na kutendewa unyama na kudhalilishwa, kinyume na sheria za kimataifa za haki za binadamu".

Mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa Marekani Antony Blinken amesema "amesikitishwa" na hatua ya jeshi kukataa kuiachilia familia ya Bazoum kama njia ya "kuonyesha nia njema".

Shirika la Human Rights Watch lilisema kuwa lilizungumza na Bazoum mapema wiki hii ambapo alielezea jinsi alivyotendewa binafsi, mke wake na mwanae kuwa ni "unyama na ukatili", HRW imesema.

Wakuu wa majeshi kutoka jumuiya ya kikanda, ECOWAS wanatarajiwa kukutana wiki ijayo mjini Accra, Ghana kujadili uwezekano wa kuingilia kijeshi kufuatia uamuzi wa jumuiya hiyo wa kupeleka kikosi cha ECOWAS nchini Niger.

Chanzo: Bbc