Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mapigano kati ya waasi wa M23 na Jeshi yasababisha wimbi jipya la wakimbizi

Mapigano Kati Ya Waasi Wa M23 Na Jeshi Yasababisha Wimbi Jipya La Wakimbizi Mapigano kati ya waasi wa M23 na Jeshi yasababisha wimbi jipya la wakimbizi

Mon, 5 Feb 2024 Chanzo: Voa

Mapigano makali kati ya waasi wa M23 na jeshi la serikali yamesababisha wimbi jipya la wakimbizi wa ndani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, vyanzo mbalimbali katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kusini vimesema Jumapili.

Kulingana na vyanzo hivyo, siku ya Ijumaa waasi wa M23 waliliteka eneo la Shasha kwenye barabara inayounganisha miji ya Goma na Bukavu.

Tangu wakati huo, mji wa Minova ulioko kusini mwa barabara hiyo unapokea wakimbizi wengi wa ndani wanaokimbia kusonga mbele kwa waasi hao, mwakilishi wa mashirika ya kiraia huko Minova Delphin Birimbi ameliambia shirika la habari la AFP.

Wakitokea katika wilaya ya Masisi huko Kivu Kaskazini, wakimbizi hao wa ndani wameomba hifadhi katika nyumba za wakazi, shule na makanisa, Birimbi ameongeza.

“Waumini hawakwenda kanisani Jumapili kwa sababu ya hofu ambayo inazidi kuongezeka na kudumaza shughuli,” amesema mwandishi wa habari wa radio ya huko Minova.

Chanzo: Voa