Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mapigano RSF na jeshi yafikisha mwaka mmoja

Sudan Kusini Drc Mapigano RSF na jeshi yafikisha mwaka mmoja

Mon, 15 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Leo ni mwaka mmoja kamili tangu kuanza kwa vita nchini Sudan, kati ya wanajeshi wa Serikali na wapiganaji wa vikosi vya RSF, mgogoro ambao umesababisha vifo vya maelfu ya raia na mamilioni kukimbilia katika nchi jirani kama Chad na Sudan Kusini.

Kwa raia wengi wa Sudan, wanataka kuona vita hii ikikoma kama anavyoeleza hapa, Ahmed Awad, mwanafunzi wa utabibu katika chuo kikuu cha Khartoum, aliyelazimika kukiùbia Sudan Kusini.

‘‘Huu ndio ujumbe wangu, lazima vita vikomeshwe, mimi sikuwa natarajia kuwa mkimbizi, tatizo kubwa tunalokabiliwa nalo ni kupata ajira.’’ alisema Ahmed Awad, mwanafunzi wa utabibu katika chuo kikuu cha Khartoum.

Kwa upande Wake, Ali Alhaji Dafalah, mjumbe wa jenerali Burhan, amesisitiza kuwa kiongozi wao yuko tayari kutoa msamaha kwa wapiganaji wa RSF ikiwa watajisalimisha.

‘‘Iwapo waasi hawa wenye silaha watakomesha uasi, tutawasamehe na tuko tayari kumkaribisha kwenye jeshi letu.’’ alieleza Ali Alhaji Dafalah, mjumbe wa jenerali Burhan.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live