Mapacha waliotimiza umri wa miaka 80 mwaka huu wameiambia BBC jinsi mama yao aliyowaficha katika miaka ambapo mapacha walikuwa wanaonekana kama laana. Ni nadra kuwapata mapacha wote hai wakiwa na umri wa miaka yao wanasema
Wakizungumza na BBC Idhaa ya Igbo nchini Nigeria mmoja Christian Odocha, alisema kuwa wakati walipozaliwa katika mji wa Isiokpo katika jimbo la Rivas, watu katika kijiji chao wanasemekana kuwa walikuwa wakiwatupa kwasababu lilikuwa ni jambo lisilofaa kwa mwanamke kujifungua watoto wawili kwa mpigo, lakini mama yao aliwalinda sana na kukataa kuwatupa.
Anasema anafurahia sana na kujivunia kuona kwamba yeye na pacha wake wameishi kwa miaka 80.
Christian ni mchungaji wa kanisa, huku pacha wake akiwa ni Mhandisi.