Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mamia za familia zilizofukuzwa Embu zalazimika kuhamia katika shule

F8bc30c9c012e1df Mamia za familia zilizofukuzwa Embu zalazimika kuhamia katika shule

Tue, 27 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Familia kutoka Makima zilipoteza makazi Jumamosi, Aprili 24, baada ya kutimuliwa na maafisa wa polisi

- Kipande cha ardhi cha ekari 66,000 ambacho wakazi hao walitimuliwa ni mali ya Mamlaka ya Maendeleo ya Mito ya Tana na Athi (Tarda)

- Familia zilizoathiriwa, ambazo sasa zimelazimika kulala madarasani, ziliwaomba wahisani kuwapa msaada wa chakula

Mamia ya familia zilizotimuliwa kutoka makazi yao huko Makima, Mbeere Kusini, kaunti ya Embu zimelazimika kutafuta makao katika shule jirani eneo hilo.

Familia kutoka vijiji vya Muthithu, Ndunguni, Twanyonyi, Kituneni, Mwanyani na Nunga zilikosa makazi Jumamosi, Aprili 24, baada ya kuondolewa kwa nguvu na maafisa wa polisi waliokuwa wamejihami kwa silaha.

Kipande cha ardhi cha ekari 66,000 ambacho wakazi hao walitimuliwa ni mali ya Mamlaka ya Maendeleo ya Mito ya Tana na Athi (Tarda). Hata hivyo, wakaazi walisema wameishi katika eneo hilo ambalo yamekuwa makazi yao kwa miongo kadhaa.

Familia zilizoondolewa sasa zinalala kwenye sakafu baridi katika shule za msingi za Muthithu, Mwanyani na Ndunguni huko Mbeere Kusini.

Taasisi hizo hata hivyo, hazina maji na vyoo vya kutosha. Shule hizo vile vile ambazo zimekuwa makazi ya waathiriwa zitafunguliwa hivi karibuni na wanafunzi kuanza tena kusoma kwa karibu wiki mbili zijazo.

Kwa sababu hiyo, familia zilizoathiriwa ziliwasihi wahisani kuwapa msaada wa chakula kabla yao "kufa na njaa".

Wakaazi wa eneo hilo wakiongozwa na mbunge wao Geoffrey King'ang'i walihusika na maafisa wa usalama katika kuendesha mapigano wakati walipokaidi maagizo ya kuondoka katika ardhi hiyo yenye mabishano.

Wakati wa operesheni hiyo, mtu mmoja alipigwa risasi na kujeruhiwa vibaya. Maafisa waliokuwa wakiendeleza oparesheni hiyo walilazimika kuwatupia vitoa machozi wenyeji waliokuwa wakiandamana.

Mbunge na wanahabari saba waliokuwa wakinakili maandamano hayo walikamatwa lakini baadaye waliachiliwa Jumapili, Aprili 25.

Wanahabari hao, kulingana na Baraza la Habari la Kenya, walikuwa Solomon Mwaniki (Standard Media Group), Dennis Fundi (Meru TV), William Moige (Standard Media Group), Josephat Mukundi, Peter Mungai (Citizen TV), Brian Malila (County FM), Mary Wangari (Coro FM), Felix Ndambuki (Athiani FM) na Dan Makenge (U- TV).

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke