Fri, 29 Sep 2023
Chanzo: Bbc
Serikali nchini Niger imesema takriban wanajeshi 12 wamefariki baada ya kushambuliwa na watu wanaoshukiwa kuwa wananmgambo wa jihadi kusini-magharibi mwa nchi hiyo.
Wizara ya ulinzi imesema wanajeshi saba waliuawa katika mapigano, wakati kikosi chao kiliposhambuliwa na mamia ya waasi waliokuwa kwenye pikipiki katika mji wa Kandadji.
Wengine watano walifariki katika ajali ya barabarani walipokuwa wakijaribu kuja kusaidia kitengo hicho.
Washirika wa ndani wa al-Qaeda na kundi la Islamic State wanafanya kazi katika eneo hilo - ambalo liko karibu na mpaka wa Mali na Burkina Faso
Chanzo: Bbc