Mambo ya msingi kuhusu rais wa mwisho mweupe wa Afrika Kusini
Hapa tumekukusanyia mambo muhimu kuhusu Rais wa zamani wa Afrika Kusini, FW de Klerk, Rais wa mwisho mweupe aliyefariki dunia leo:
- Alikuwa Mkuu wa nchi kati ya Septemba 1989 na Mei 1994.
- Hakuwahi kuviwekea vikavyo vyama vya ukombozi ikiwemo African National Congress pamoja na mashirika mengine ya kupinga ubaguzi wa rangi mnamo Februari 1990.
- Alimwachia huru Nelson Mandela na wafungwa wengine wa kisiasa wakati huo huo.
- Alishinda Tuzo ya Amani ya Nobel na Mandela mwaka 1993 kwa kuongoza kipindi cha mpito cha kukomesha utawala wa wachache.
- Alikabidhi madaraka kwa Rais Mandela baada ya uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia nchini Afrika Kusini mwezi Aprili 1994.
- Alihudumu chini ya Mandela kama Naibu Rais.
- Kuondoka serikalini mwaka 1996 baada ya tofauti kubwa juu ya sura ya baadaye ya serikali.
- Alikosolewa vikali sana kwa kukataa kukiri mwaka 2020 kwamba ubaguzi wa rangi ulikuwa uhalifu dhidi ya ubinadamu.
A white hearse escorted by traffic police has just left former head of state FW De Klerk's home in Cape Town. @TeamNews24 pic.twitter.com/rYQHn12ibb
— Jenni Evans (@itchybyte) November 11, 2021