Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mama wa watoto 10 asema mumewe anamlazimisha azae watoto 22

D3cfb5e631495467 Mama wa watoto 10 asema mumewe anamlazimisha azae watoto 22

Mon, 26 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mwanamke mmoja kutoka Kakamega ambaye ni mama wa watoto 10 kwa sasa ana mimba ya mwanawe wa 11Kulingana na Gentrix Wekesa, mume wake anafikiria kuwa watoto wachache watamgeuza kuwa kichekoPia anaamini kuwa kuzaa watoto wengi kunasaidia wakati wengine watakuwa watukutu hawawezi kuathiri maisha ya wengine kwa sababu ni wengi

Mama wa watoto 10 kutoka kaunti ya Kakamega amefichua kuwa mume wake amekataa kukubali mpango wa kupanga uzazi akishikilia kuwa anataka kuwa na watoto 22.

Mama huyo mwenye umri wa miaka 30, kwa jina Gentrix Wekesa kutoka kijiji cha Navakholo, anatarajia kupata mtoto wake wa 11, na alisema mume wake alikataa kutumia mpango wa kupanga uzazi kwa sababu ya tamaduni.

Akizungumza na TV 47, mama huyo mwenye wasiwasi alisema:

"Mimi huzaa hawa watoto kila mwaka. Punde ninapo anza hedhi zangu, napata mtoto mwingine, mdogo bado hajafikisha mwaka mmoja."

Read also

Ubinafsi wa baadhi ya wanasiasa unahatarisha kwenye mapambano dhidi ya COVID-19

Gentrix , ambaye ndiye anategemewa kwenye familia hiyo alisema, amechoshwa na mzigo wa kuwalea watoto hao.

"Ilifikia wakati mmoja ambapo mmoja wa watoto aliwacha shule akiwa Darasa la Saba kwa sababu walishinda wakimfukuza karo ama sare, sikuwa na la kufanya. Wa pili pia amewacha shule. Kwa hivyo nilimpeleka mahali asaidie mtu kumchungia ng'ombe na wakati analipwa ananisaidia kuwalea watoto wengine." alisema.

Mume wake, Anthony Wekesa, pia amemzuia dhidi ya kutumia dawa za kupanga uzazi.

Kulingana naye, hii ni dhana potovu ya kigeni na watoto wachache watamgeuza kuwa kicheko.

Aliwahi kujaribu kutumia dawa za kupanga uzazi lakini wakati alifika nyumbani, mume wake alimrejesha hospitalini atolewe.

"Bora anizalie idadi ya watoto ambao mimi nataka. Wanatakiwa wawe watoto,'' alisema Anthony.

Gentrix aliongezea kuwa mume wake anataka wazae watoto wengi ili wawasaidie katika maisha yao ya usoni.

Mrembo mwenye umri wa miaka 25 azaa watoto 9Kwingineko mwanamke mmoja mwenye miaka 25, nchini Mali amejifungua watoto tisa na kuweka historia ya kuwa mmoja wa wanawake duniani kuzaa pacha tisa.



Read also

Nandi: Seneta Cherargei Amtambulisha Kuria kwa Wenyeji Asema Anatosha Kuwa Naibu Rais

Kulingana na Wizara ya Afya ya Mali, mama huyo aliyetambuliwa kama Halima Cisse alikuwa anatazamiwa kuzaa watoto saba lakini uchunguzi wa ultrasound haukutambua kwamba alikuwa na watoto wengine wawili zaidi tumboni.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke