Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mama wa miaka 32 azoa alama ya B+ KCSE 2020 baada ya kuwacha shule 2006

167130317336d0cd Mama wa miaka 32 azoa alama ya B+ KCSE 2020 baada ya kuwacha shule 2006

Tue, 11 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Purity Nkatha aliwacha shule mwaka 2006 na kuenda kuishi na halati yake Malindi ambapo alianza kufanya kazi katika mabaa na mahoteli

- Mnamo 2014, alikutana na mwanaharakati mtandaoni na baada ya kusemezana, mwanaharakati huyo alikubali kumlipia karo ya shule

- Sasa anasherehekea baada ya kupata alama ya B+ kwenye mtihani wa KCSE 2020

Mnamo mwaka 2006, Purity Nkatha alidhania kwamba ndoto zake zimevunjika wakati vita vya nyumbani vilimfanya kuwacha shule na kuenda kuishi na halati yake.

Alikuwa akisoma katika Shule ya Sekondari ya Wavulana na Wasichana ya Kisima, kaunti ya Meru wakati mama yake alimpeleka kuishi na halati yake Malindi.

Akizungumza na The Standard, mama huyo wa mtoto mmoja sasa anasherehekea baada ya kupata alama ya B+ kwenye Mtihani wa Kidato cha Nne (KCSE) 2020 akikumbuka alivyoanza kufanya kazi katika mabaa na mahoteli kujikimu.

Mnamo 2014, alianza kumfuata mwanaharakati Irene Kendi, ambaye alikuwa anapigania haki za wanawake na wasichana mtandaoni na aliguswa na kazi yake.

Kisha alimtumia ujumbe na baada ya kusemezana, Kendi alikubali kumlipia karo ya shule na 2018 alirejea shuleni kwa mara ya kwanza tangu 2006.

"Niliolewa 2013 na kupata mtoto 2014. Nilirudi shule 2018 wakati Bi Kendi, ambaye sijawahi kukutana naye alijitolea kunirejesha shule.Kendi alikuwa analipa karo naye mume wangu aligharamia nauli na mahitaji yangu mengine," alisema.

Na sasa bidii ya mwanafunzi huy mwenye umri wa miaka 32 ambaye alikuwa anasomea katika Shule ya Upili ya Magumoni, haraka Nithi imezaa matunda.

Nkatha alipata A katika somo la Dini, A-Somo la Biashara, A-Historia na B+ kwenye Kiswahili. Na anatazamia kosemea ualimu ama uuguzi.

Waziri wa Elimu George Magoha alitangaza matokeo hayo majuma mawili baada ya watahiniwa 741, 161 kumaliza mitihani yao Aprili 21, 2021.

Kati ya watahiniwa hao 747,161, 366,834 walikuwa wasichana na wengine 380,327 wavulana.

Kulingana na matokeo hayo, yaliyotangazwa Jumatatu, Mei 10, watahiniwa 893 walipata alama ya A huku 143, 140 wakipata alama zitakazowawezesha kuingia moja kwa moja katika Vyuo Vikuu.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke