Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mama mwenye miaka 37 arudia Kidato cha 4 baada ya kupata C- KCSE 2020

531ff213ea724c33 Mama mwenye miaka 37 arudia Kidato cha 4 baada ya kupata C- KCSE 2020

Mon, 17 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Ann Otindo alisema ana ndoto ya kuwa mwalimu na hivyo alirejea shuleni akiwa na matumaini ya kupata alama ya C+ na kuendelea

- Mama huyo wa watoto watano aliwacha shule akiwa Kidato cha Kwanza na kuolewa na Peter Wamalwa

- Baada ya miaka kadhaa katika ndoa, aliamua kurejea shuleni kutimiza ndoto yake

Mama mwenye umri wa miaka 37, ameamua kurudia Kidato Cha Nne baada ya kupata gredi ya chini kwenye Mtihani wa Kitaifa wa Kidato cha Nne(KCSE) 2020 kinyume na matarajio yake.

Katika matokeo hayo yaliyotangazwa na Waziri wa Elimu George Magoha Jumatatu, Mei 10, Ann Otindo kutoka eneo bunge la Kabuchai, kaunti ya Bungoma alipata alama ya C-.

Akizungumza na TV47, mama huyo wa watoto watano alisema ana ndoto ya kuwa mwalimu na hivyo alirejea shuleni akiwa na matumaini ya kupata alama ya C+ na kuendelea.

"Niliamua kurejea shuleni kwa sababu bila amsomo, hauweziz kuishi amisha mazuri," alisema Otindo.

Mama huyo aliwacha shule akiwa Kidato cha Kwanza na kuolewa na Peter Wamalwa

Mnamo 2017, akiwa na umri wa miaka 34, aljiunga na Shule ya Sekondari ya Marafiki ya Musokho ambapo alifanya mtihani wake mwaka 2021.

"Kwa wanawake wote ambao wanataka kurudi shule, wacha niwashauri kuwa ndoa si taaluma," aliongezea.

Bidii yake ilimgusa mbunge wa eneo hilo Majimbo Kalasinga ambaye aliahidi kumlipia karo ya mwaka mzima na kuwatunza wanawe.

Katika matokeo hayo, Simuyu Robinson Wanjala wa Shule ya Upili ya Murang'a ndiye aliyeibuka wa kwanza na alama ya A na pointi 87.334 l

Alifuatwa na mwanafunzi wa Shule ya Agoro Sare Wesonga Allan na alama ya A yenye pointi 87.173, sawia na Sharon Chepgeno Terer kutoka Shule ya Kenya High aliyeorodheshwa wa tatu.

Muriasi Rob Ongare kutoka Shule ya Alliance High aliibuka wa nne na alama 87.173, huku Mbugua Esther kutoka Shule ya Kenya High akimalizia orodha ya wanafunzi tano bora na A ya pointi 87.113.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke