Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mama ashtuka na kufariki "akihofia kukamatwa na polisi" kwa kutovaa maski

6aa705dd141a8885 W Mama ashtuka na kufariki "akihofia kukamatwa na polisi" kwa kutovaa maski

Thu, 3 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mama huyo alishtuka na kuzirai baada ya habari kusambaa kwamba maafisa wa polisi walikuwa wanawakamata watu ambao hawajavaa maski

- Marehemu alianza kusakanya maski kwenye mkoba wake lakini hakuwa anapata na hata kutaka kutoroka lakini swahiba wake alimuomba atulie

- Licha ya kufanikiwa kupata barakoa yake, alianza kulalamika kuwa moyo wake ulikuwa unapiga kwa kasi na kuanza kukohoa damu

- Alikimbizwa katika hospitali ya kibinafsi ambapo alithibitishwa kufariki

Dada mmoja kutoka kijiji cha Kwa Mwango, kaunti ya Kilifi ameaga dunia kwa kile kimedaiwa kuwa alishtuka kufuatia msako wa polisi dhidi ya watu ambao hawakuwa wamevaa barakoa Jumatatu, Mei 31.

Kwa mujibu wa Taifa Leo, mama huyo alishtuka na kuzirai baada ya habari kusambaa kwamba maafisa wa polisi walikuwa wanawakamata watu ambao hawajavaa maski.

"Alikuwa ameniambia niandamane naye kuchukua pesa alizokuwa anawadai wateja wake eneo la Kiwandani. Tulipokuwa tunarudi nyumbani tulikutana na kijana ambaye alitwambia tuvae maski kwa sababu polisi walikuwa wanaeleka upande wetu," alisema swahiba wake Nelvina Nzai.

Kijana huyo alikuwa anawatoroka polisi kwa sababu hakuwa amevaa maski.

Kisha marehemu alianza kusakanya maski kwenye mkoba wake lakini hakuwa anapata na hata kutaka kutoroka lakini swahiba wake alimuomba atulie.

Licha ya kufanikiwa kupata barakoa yake, alianza kulalamika kuwa moyo wake ulikuwa unapiga kwa kasi na kuanza kukohoa damu.

Alipandishwa pikipiki na kukimbizwa hospitalini ambapo alithibitishwa kufariki.

Familia yake ilisema marehemu alikuwa akiugua ugonjwa wa kisukari na kulaumu polisi kwa ukatili wao ambao unawafanya raia kuwaogopa bila kuwa na makosa.

Kamanda wa polisi wa Kaunti Ndogo ya Kilifi Kaskazini, Jonathan Koech alishauri familia hiyo iwasilishe malalamishi yao ili uchunguzi ufanywe.

Koech alisema kuwa upasuaji wa maiti utafanywa kwanza kuthibitisha chanzo cha kifo.

Aliongezea kuwa polisi wanataka kufanya kazi yao kwa kuheshimu haki za biandamu na kumtaka yote aliye na malalamishi ya kudhulumiwa apige ripoti.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke