Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mama anaswa kwenye kamera akiiba sadaka kanisani

82ff6da4b0a7fd10 Mama anaswa kwenye kamera akiiba sadaka kanisani

Mon, 5 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Katika video iliyochapishwa kwenye mtandao wa kijamii mwanamke huyo anaonyeshwa akiwa ndani ya chumba kimoja na kikapu cha sadakaKisha alichukuwa pesa alizohitaji na kuingiza ndani ya sidiria yakeBaada ya kuhisi ameridhika na kiasi hicho cha pesa, aliondoka haraka kwenye chumba hicho kabla ya kukamatwa

Ama kweli kuna watu wa viatu yani watu wanakosa aibu kabisaa hadi wanamuibia Mungu. Video moja imesambaa kwenye mtandao wa kijamii ikimuonyesha mshirika wa kanisa lisilojulikana akiiba pesa kutoka kwenye kikapu cha sadaka.

Katika video hiyo iliyochapishwa kwenye ukurasa wa Instagram na yabaleftonline, mnamo Ijumaa, Julai 2, mwanamke huyo anaonyeshwa akiwa ndani ya chumba kimoja na kikapu cha sadaka kisha alichukuwa pesa alizohitaji na kuingiza ndani ya sidiria yake.

Baada ya kuhisi ameridhika na kiasi hicho cha pesa, aliondoka haraka kwenye chumba hicho kabla ya kukamatwa.

Tazama video hiyo hapa:

Katika taarifa tofauti ya Tuko.co.ke, Mhubiri anayezingirwa na utata James Ng'ang'a alipata pigo kubwa siku ya Jumanne, Juni 15, baada ya kushindwa kuzuia wanahabari kupeperusha kesi inayomkabili ya ulaghai wa KSh 3.6 milioni.

Pasta Ng'ang'a anatuhumiwa kupokea KSh3.6 milioni kwa njia ya udanganyifu mnamo Aprili 6, 2016 kutoka kwa mwanabiashara Wickson Njoroge Mwathe akidai atamkodisha nyumba katika mtaa wa Karen Estate, Nairobi.

Kwingineko, Papa Francis anatazamiwa kufanyiwa upasuaji wa kutibu tatizo kwenye utumbo wake mpana saa chache baada ya kiongozi huyo kuhudhuria maombi ya Angelus katika Kanisa la St Peter's Square.

Taarifa hii inakujia wiki moja baada ya Papa kuomba umma kumfanyia maombi spesheli “Ninawaomba kumuombea Papa katika njia spesheli. Papa anahitaji maombi yenyu,” alisema kama alivyonukuliwa na The Guardian.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke