Serikali ya Malawi imetuma maombi kwa Bingwa wa zamani wa ndondi wa uzito wa juu duniani Mike Tyson kuwa balozi wa chapa ya bangi ya Malawi.
Katika barua hiyo ya tarehe 1 Novemba, Waziri wa Kilimo, Lobin Lowe, alibainisha kuwa kuhalalishwa kwa Bangi mwaka 2020 kumeunda fursa kwa madhumuni ya dawa na viwanda na pia kumetoa fursa kwa Malawi kuzalisha fedha za kigeni.
"Pamoja na faida hizi zote zinazoonekana, Malawi inaweza isiende peke yake kwani sekta hiyo ni ngumu inayohitaji ushirikiano. Kwa hivyo ningependa kukuteua, Bw Mike Tyson, kama balozi wa Tawi la Bangi la Malawi,” Lowe alisema.
Alisema Jumuiya ya Bangi ya Merika inafanikisha mpango huo na Tyson.
Taarifa za vyombo vya habari zinaeleza kuwa Tyson alitarajiwa kuwepo nchini wiki iliyopita lakini safari hiyo iliahirishwa kwa kuwa Wizara bado haijakamilisha maandalizi ya shughuli zake nchini Malawi.