Thu, 11 Apr 2024
Chanzo: Bbc
Mamlaka nchini Comoro zimesema makumi ya wafungwa wametoroka katika gereza moja katika mji mkuu Moroni, kwa kutembea wakipita tu kwenye lango kuu.
Mwendesha mashtaka wa umma visiwani humo, Ali Mohamed Djounaid, alisema wafungwa 38 walitoweka katika Gereza la Moroni, kubwa zaidi katika visiwa hivyo.
Aliwalaumu walinzi waliozembea. Msemaji wa serikali alisema kutoroka kunaonekana kuwa kulipangwa mapema.
Chanzo: Bbc