Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Makumi ya raia Afrika Kusini wakamatwa wakiandamana kupinga kufungwa kwa Zuma

E6b274345a14bfb2 Makumi ya raia Afrika Kusini wakamatwa wakiandamana kupinga kufungwa kwa Zuma

Mon, 12 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Maduka huko Johannesburg yaliporwa usiku na sehemu ya barabara kuu ya M2 ilifungwa wakati maandamano mengine yalipobadilika kuwa ya vuruguMwili wa mwanamume mwenye umri wa miaka 40 ulipatikana katika moja ya maduka ambayo yaliteketezwa moto mwishoni mwa wiki, kulingana na ripoti ya polisiZuma, mpiganaji mashuhuri dhidi ya ubaguzi wa rangi, bado ni maarufu licha ya madai ya ufisadi yanayomkabiliMaandamano dhidi ya kufungwa jela kwa rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma yalisambaa kutoka eneo alikozaliwa hadi jijini Johannesburg Jumapili, Julai 11.

Maduka huko Johannesburg yaliporwa usiku na sehemu ya barabara kuu ya M2 ilifungwa wakati maandamano mengine yalipobadilika kuwa ya vurugu.

Polisi wanasema watu 62 wamekamatwa kwa kuhusika na ghasia tangu Zuma alipofungwa jela Jumatano wiki iliyopita.

Mwili wa mwanamume mwenye umri wa miaka 40 ulipatikana katika moja ya maduka ambayo yaliteketezwa moto mwishoni mwa wiki, kulingana na ripoti ya polisi.

Read also

Mombasa: Mganga Akamatwa na Kupokonywa KSh18M, Magari ya Kifahari ya KSh 30M

Mnamo Jumapili, Rais Cyril Ramaphosa alitaka utulivu kurejea, na wakati huohuo akiwataka waandamanaji kuandamana kwa amani.

"Watu wametishwa, na wengine wameumizwa," Ramaphosa alisema.

Zuma anatumikia kifungo cha miezi 15 kwa kudharau korti baada ya kushindwa kutoa ushahidi wakati akichunguzwa kuhusiana na madai ya ufisadi wakati wa kipindi chake akiwa rais kutoka 2009-2018.

Maandamano yalianza mara tu baada ya kukamatwa kwake wiki iliyopita katika mkoa wa kwao KwaZulu-Natal.

Maduka huko KwaZulu-Natal na mkoa wa Gauteng, ilipo Johannesburg, yamebaki kufungwa Jumatatu, Julai 12 kwa sababu za usalama, taarifa kutoka nchini humo zimesema.

Zuma amekanusha madai kwamba ufisadi ulienea chini ya uongozi wake, na alikataa kushiriki katika uchunguzi ambao ulianza wiki za mwisho za uongozi wake.

Pia amepinga adhabu yake ya sasa, akisema katika sehemu ya utetezi wake kuwa atakuwa katika hatari ya kuambukizwa COVID-19 akiwa gerezani. Korti inatarajiwa kusikiliza malalamiko yake leo.



Read also

Caroline Kangogo: DCI Yashindwa Kufuatilia Nyayo za Mshukiwa Baada ya Kuzima Simu

Zuma, mpiganaji mashuhuri dhidi ya ubaguzi wa rangi, bado ni maarufu licha ya madai ya ufisadi yanayomkabili.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke