Wakazi wa maeneo ya kifahari jijjini Nairobi nchini Kenya wamemuandikia Naibu Rais wa taifa hilo na kulalamikia kuhusu kelele zinazotoka nyumbani kwake.
Makamu wa rais William Ruto amekuwa akifanya mikutano ya kisiasa nyumbani kwake huko Karen.
Wakazi sasa wanasema kwamba kelele kutoka mikutano hiyo ya kisiasa zinawadhuru.
Pia wamelalamikia kuhusu usalama wao , ikiwemo wizi wa mabavukatika barabara inayoelekea katika nhyumba ya kiongozi huyo na watu wanaojifanya kuwa wageni wa nyumba hiyo ya makamu wa rais, alisema mwenyekiti wa Muungano wa wakaazi wa eneo hilo James Hirst.
Wageni walioegesha magari yao nje pia wameshtumiwa kwa kusababisha trafiki katika njia hiyo. Familia Tajiri huishi katika eneo la Karen ambapo kuna usalama wa saa 24.
Hosted a forum for UDA aspirants from Bomet, Kericho, Nandi, Uasin Gishu, Turkana, West Pokot, Baringo and Elgeyo Marakwet, Samburu and Trans Nzoia counties at Karen, Nairobi County. pic.twitter.com/dhSXx3mkRv
— William Samoei Ruto, PhD (@WilliamsRuto) November 9, 2021