KWA mara ya kwanza katika historia, Misri imewaapisha wanawake 98 kuwa Majaji katika moja ya vyombo vikuu vya idara ya mahakama nchini humo, inayofahamika kama Baraza kuu la serikali.
Majaji hao waliapishwa mbele ya jaji mkuu wa baraza hilo katika hafla iliyofanyika katika mji mkuu Cairo jana Jumanne, uapisho huu unakuja miezi kadhaa baada Rais Abdul Fattah Al-Sisi kuwataka wanawake wajiunge na vyombo vikuu viwili vya mahakama, baraza na Mashtaka ya Umma.
Tangu kuanzishwa kwake mnamo 1946, baraza la serikali limekuwa likiwateua wanaume pekee kuwa majaji na kukataa maombi ya wanawake, katika miaka iliyopita, wanawake walipinga maamuzi ya baraza, hilo wakisema kuwa wanabaguliwa.