Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maiti yagoma kuingia kwenye jeneza Kenya

0fgjhs71aahojklj4 Maiti yagoma kuingia kwenye jeneza Kenya

Fri, 6 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Waombolezaji waliofika katika boma moja eneo la Kilingili, Vihiga waliachwa midomo wazi baada ya mwili wa marehemu kukataa kuingia ndani ya jeneza hadi ulipovishwa viatu vipya alivyokuwa amenunua.

Duru zinaarifu kwamba jeneza lililetwa kisha jamaa na marafiki wa mwenda zake walimkaribia na kuubeba mwili wake kwa makini kuuweka ndani ya jeneza.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Taifa Leo walishtuka baada ya mwili huo kuanza kufura na jeneza kuonekana kuwa dogo.

Inasemekana kwamba waliotwikwa jukumu hilo waliamua kulipanua jeneza lakini walipojaribu kuuweka mwili huo ndani ya sanduku safari hii ulirefuka.

“Lazima kuna mtu marehemu hamtaki hapa. Haya mambo hayawezi kufanyika bila sababu,” jamaa mmoaj alisikika akisema.

Waombolezaji walipoarifiwa kuhusu kisa hicho walibaki wamepatwa na mshtuko.

“Kama amekataa kuingia jenezani hata kaburini basi pia atakataa. Lazima kuna mchawi hapa,” mwombolezaji mmoja alisika akisema.



Read also

Moto Gikomba: Wafanyabiashara Katika Soko la Gikomba Wapata Hasara

Penyenye za kijijini zilisema kwamba ilibidi wazee wa kijijini waliitwa kutegua kitendawili hicho.

“Watu wote watoke nje,” wazee waliamuru.

Inaarifiwa kwamba wazee walipoachwa chumbani humo walianza kumtandika viboko marehemu.

“Usipokubali kuingia ndani ya jeneza tutakutupa kama mbwa. Ingia humu mara moja,” sauti ya mzee mmoja ilisikika ikiamuru kutoka chumbani.

Semasema zinaarifu kwamba baada ya dakika tano za adhabu kali mlango ulifiinguliwa na wazee hao wakamwita mke wa marehemu.

“Nimesikia sauti ya marehemu ikiniambia kwamba avishwe viatu vyake alivyonunua juzi,” mke wa marehemu alisema.

Viatu hivyo vililetwa haraka na mwenda zake akavishwa na baada ya hapo waliokuwa wakiutia mwili wake ndani ya jeneza waliitwa kuendelea na shughuli hiyo.

Duru zinasema kila mmoja katika mazishi hayo alibaki mdomo wazi kwani mwili uliingia jenezani bila tatizo lolote.

“Marehemu hakutaka kuacha viatu vyake nyuma,” muombolezaji mmoja alisikika akisema.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Read also

Jonathan Mukundi: Taarifa Zaidi Zaibuka Kuhusu Mauaji ya Philomena Njeri Kiambu

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke