Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mahakama yazuia polisi kumtia nguvuni Linturi kufuatia tuhuma 37 za uhalifu

38e39d516fa34a13 Mahakama yazuia polisi kumtia nguvuni Linturi kufuatia tuhuma 37 za uhalifu

Tue, 11 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mahakama Kuu imewazuia polisi kumkamatwa Seneta wa Meru Linturi aliyehusishwa na tuhuma 37 za ulaghai.

Mnamo Jumanne, Mei 11 Jaji Weldon Korir alizuia polisi na Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) kumkamata mwanasiasa huyo.

Linturi, ambaye alipaswa kufunguliwa mashtaka katika mahakama kuu ya Milimani Jumatano, alielekea kotini kupingwa kukamatwa kwake.

Uamuzi wa hivi punde unawadia siku chache baada yake kuhojiwa katika Idara ya Upelelazi mnamo Aprili 28.

Kulikuwa na madai kwamba alikuwa amekamatwa kwa sababu ya msimamo wake kuhusu Mswada wa Maridhiano (BBI), madai ambayo yalisababisha mabishano makali katika Seneti.

Seneta Aaron Cheruiyot alikuwa ameambia Seneti kwamba alikuwa amepokea simu kutoka Linturi akimjulisha amekamatwa na maafisa wa DCI.

Suala hilo lilimfanya Spika kuahirisha kikao maalum ambacho kiliandaliwa kujadili mchakato huo.

Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i alithibitishia Kamati ya Seneti kuhusu Usalama kuwa kukamatwa kwa Seneta huyo wa Meru kulikuwa halali.

Akifika mbele ya kamati hiyo Ijumaa, Mei 7, Matiang'i alifichua kuwa Linturi na wenzake wamekuwa wakichunguzwa na Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka ya Umma(ODPP).

Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka ya Umma Noordin Haji aliidhinisha kushtakiwa kwa mwanasiasa huyo pamoja na Emily Nkirote Buantai uchunguzi ulipokamilishwa Februari 2021.

Baadhi ya mashtaka ni kutoa taarifa za uwongo kumhusu mtu aliyeajiriwa na Tume ya Utumishi wa Umma (PSC), utapeli, udanganyifu, kutoa stakabadhi ghushi na kupata pesa kwa njia ya udanganyifu.

Pia watakabiliwa na mashtaka kuhusu kughushi stakabathi za kesi ambayo ni kinyume cha sehemu ya 348 ya katiba.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke