Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mahakama yamuagiza Rais Kenyatta kuteua majaji wengine 6

Cbeae4686ef5e9fd Mahakama yamuagiza Rais Kenyatta kuteua majaji wengine 6

Fri, 22 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Ijumaa yameangazia taarifa za amri ya mahakama ambayo ilimwagiza Rais Uhuru Kenyatta kuwateua majaji sita waliopendekezwa na tume ya huduma za mahakama JSC.

Kumekuwa na utata kuhusu majaji hao ambao Rais alidinda kuwateua akisema ujasusi una ripoti mbaya kuwahusu.

1. Star

Gazeti hili lina taarifa kuhusu siasa za 2022 ambapo kinara wa ANC Musalia Mudavadi amesema anamtafuta Rais Uhuru ili kujua wazi iwapo chaguo lake la 2022 ni kinara wa ODM Raila Odinga.

Alisema kuungwa mkono na serikali inaweza ikawa bahati au kumletea masaibu kwenye uchaguzi wa 2022.

Gazeti hili limeendelea na taarifa hizo huku likichapisha semi za naibu rais William Ruto na wandani wake ambao walisema Raila ni 'Project ya Deep State'.

2. People Daily

Taarifa kuu hapa ni kuhusu amri ya mahakama kwa Rais kuwateua majaji sita ndani ya siku kumi na nne zijazo.

Mahakama ilisema Rais asipofanya hivyo, basi sheria itatambua kuwa majaji hao tayari wameteuliwa na wataanza kuchapa kazi.

Uamuzi huo ulitolewa na majaji watatu wa mahakama ya Juu Alhamisi Oktoba 21 ambapo walisema siku 14 zikikamilika Jaji Mkuu na JSC wanafaa kuapisha majaji 6.

JSC iliwateua majaji 40 iliopendekeza wapandishwe ngazi lakini Kenyatta akawaacha sita akisema ana ripoti za ujasusi kuwahusu.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke