Fri, 25 Jun 2021
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke
Mahakama imeshikilia kuwa Naibu Gavana wa Nairobi Ann Kananu alichaguliwa kihalali na kwa mujibu wa katiba.
Kwenye uamuzi uliotolewa na majaji watatu, mahakama ilisema aliyekuwa gavana Mike Sonko alikuwa amemteua Kananu lakini hakuwa na uwezo wa kuondoa jina lake baadaye.
Majaji hao pia walisema IEBC haikufanya kosa lolote kwa kukosa kuitisha uchaguzi mdogo baada ya kubanduliwa kwa Gavana Mike Sonko kwani kisheria mtu aliyeteuliwa naibu gavana huchukua usukani.
Uamuzi huo ndio msumari wa mwisho kwenye jeneza la Sonko kwani sasa Kananu ataapishwa kuwa gavana rasmi wa tatu wa kaunti hiyo.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke