Majaji wa Mahakama ya Rufaa ya Umoja wa Mataifa, wameamuru kuwa mshukiwa wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda Félicien Kabuga aachiwe na kwamba kesi ya uhalifu wa kivita dhidi yake isitishwe kwa muda usiojulikana.
Majaji wa Mahakama ya Rufaa ya Umoja wa Mataifa, wameamuru kuwa mshukiwa wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda Félicien Kabuga aachiwe na kwamba kesi ya uhalifu wa kivita dhidi yake isitishwe kwa muda usiojulikana. Mahakama ya uhalifu wa kivita ya Umoja wa Mataifa mapema mwenzi Juni iliamua kuwa Kabuga hafai kufikishwa mahakamani kutokana na ugonjwa wa akili lakini walipendekeza taratibu mbadala zifanyike.