Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mahakama yaamuru Zuma arudishwe tena gerezani

Zuma?fit=1200%2C794&ssl=1 Jacob Zuma, Rais wa zamani wa Afrika Kusini

Wed, 15 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mahakama ya Afrika Kusini imeamua kuwa rais wa zamani Jacob Zuma anapaswa kurejea gerezani, ikisema kuwa msamaha wa kimatibabu aliopewa awali ulikuwa"kinyume cha sheria".

Muda aliokaa nje ya gereza haupaswi kuhesabiwa katika hukumu yake ya miezi 15 ,mahakama ya Pretoria aliamua.

Zuma aliachiliwa huru Septemba 5, kwa hali ya kiafya ambayo haikufichuliwa.

Alikuwa amefungwa gerezani kwa kushindwa kuhudhuria uchunguzi kuhusiana na na ufisadi wakati wa urais wake.

Bw Zuma mwenye umri wa miaka 79 alijisalimisha kwa polisi mwezi Julai, lakini kifungo chake, ambacho hakikutarajiwa kiliibua maandamano na uporaji.

Zaidi ya watu 300, wengi wao wakiwa ni kutoka katika ngome ya Zuma ya jimbo la KwaZulu-Natal , walikufa katika maandamano hayo ya ghasia.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live