Wilson Macharia alituzwa kima hicho cha pesa baada ya kushtaki Safaricom kwa kile alitaja kama kukiukwa kwa haki zake Macharia alisema alinyimwa nafasi ya kuhudumu katika kampuni hiyo kwa msingi wa kukosa vifaa vya kumuwezesha kufanya kaziKatika kujitetea, Safaricom ilisema mlalamishi alipewa nafasi kwenye mahojiano
Mahakama Kuu jijini Nairobi imeamuru kampuni ya mawasiliano ya Safaricom kumlipa mwanamume kipofu KSh 6 milioni kwa kukosa kumuajiri.
Wilson Macharia alituzwa kima hicho cha pesa baada ya kushtaki Safaricom kwa kile alitaja kama kukiukwa kwa haki zake.
Macharia alisema alinyimwa nafasi ya kuhudumu katika kampuni hiyo kwa msingi wa kukosa vifaa vya kumuwezesha kufanya kazi.
Katika kujitetea, Safaricom ilisema mlalamishi alipewa nafasi kwenye mahojiano.
Read also
Mwanafunzi wa Maseno School Aaga Dunia Baada ya Kuumwa na Kichwa
Macharia, hata hivyo alisema kuwa licha ya kualikwa kutia saini mkataba, alinyimwa kazi hiyo baada ya kuagizwa kutumia kipatakilishi yake.
“Nimetambua kuwa sababu za mshtakiwa (Safaricom) zilitolewa kwa mlalamishi wakati imechelewa. Mshtakiwa alifahamu fika kuanzia mwanzo kuwa kazi ya mlalamishi inahitaji mashine, japo walimpitiza kwenye utaratibu wote," aliamua Jaji Makau.
Macharia alikuwa ametuma maombi ya nafasi ya huduma kwa wateja mnamo Agosti 2016 baada ya Safaricom kutangaza kuwa wazi.
Tangazao hilo lilimtaka Mkenya yeyote kutuma maombi bila kujali uraia, rangi, jinsia, kabila, ulemavu na umri.
Macharia na watu wengine walemavu walikuwa miongoni mwa walioitwa kuhojiwa.
Alipita mahojiano hayo ya kazi na kualikwa kutia saini mkataba wake wa ajira mnamo Julai 2017 lakini kampuni hiyo ilisema alialikwa kimakosa.
Wakati alijaribu kutafuta sababu, kampuni hiyo ilidinda kuzungumzia suala hilo.
Mfanyakazi mwingne wa Safaricom alipwa KSh14.6 milioniKatika kesi nyingine, Jaji wa Mahakama ya Leba na Ajira, Maureen Onyango mnamo Marchi 2020, aliamuru Safaricom kumlipa mfanyakazi wake wa zamani KSh 14.6 milioni kwa kumfuta kazi kimakosa.
Read also
Watu 45 Wauawa Wakishinikiza Kuachiliwa Huru kwa Rais wa Zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma
Uamuzi huo ni kufuatia malalamishi yaliyowasilishwa na aliyekuwa mkurugenzi wa huduma za watej Pauline Wangeci Warui ambaye alikuwa amehudumu katika kampuni hiyo kwa miaka saba.
READ ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.