Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mahakama ya Rufaa yamwondoa Rais Kenyatta kwenye kesi ya kuapisha majaji sita

B0d681a7bb68cec0 Mahakama ya Rufaa yamwondoa Rais Kenyatta kwenye kesi ya kuapisha majaji sita

Mon, 1 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mahakama ya Rufaa imesitisha kwa muda maagizo ya Mahakama ya Juu yaliyomtaka Rais Uhuru Kenyatta kuteua majaji sita aliowaacha kwenye orodha iliyopendekezwa na JSC ndani ya siku 14.

Mahakama imesitisha agizo hilo hadi Novemba 19 wakati mahakama hiyo ikitarajiwa kuamua iwapo agizo lililotolewa kwa Rais Kenyatta litabatilishwa. Majaji sita walioachwa katika uteuzi huo ni Aggrey Muchelule, George Odunga, Weldon Korir na Joel Ngugi.

Akitoa uamuzi huo wakili wa Rais Kenyatta Waweru Gatonye alisema agizo hilo la mahakama huenda likazua misukosuko na kuzorotesha uhusiano kati ya Ikulu na afisi ya Jaji Mkuu.

Mahakama ilisitisha agizo hilo hadi Novemba 19 wakati mahakama hiyo ikitarajiwa kuamua iwapo agizo lililotolewa kwa Rais Kenyatta litabatilishwa.

"Kwa kuzingatia hali ngumu ya maswala yanayohusika, tutatoa kisigino cha muda tunapotayarisha uamuzi. Tunahisi kama korti tunahitaji kutoa maswala fulani ambayo hayawezi kufanywa mara moja," walisema majaji.

Majaji Roselyn Nambuye, Imaana Laibuta na Wanjiru Karanja walitoa uamuzi huo baada ya mawasilisho kutoka kwa Mwanasheria Mkuu Kihara Kariuki, mtetezi wa rais na Taasisi ya Katiba.

Katika wasilisho lake, wakili wa Rais Kenyatta Waweru Gatonye alisema agizo hilo la mahakama huenda likazua misukosuko na kuzorotesha uhusiano kati ya Ikulu na afisi ya Jaji Mkuu.

“Nimesikitishwa na uamuzi mzima na tangu sasa nimewasilisha na kutoa notisi ya kukata rufaa. Isipokuwa uamuzi na maagizo ya Mahakama Kuu yatasitishwa, rufaa iliyokusudiwa haitatumika,” zilisema hati za mahakama.

Majaji sita walioachwa katika uteuzi huo ni Aggrey Muchelule, George Odunga, Weldon Korir na Joel Ngugi. Hakimu mkuu Evans Makori na msajili wa Mahakama Kuu Judith Omange pia waliachwa nje.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke