Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mahakama kuamua matokeo ya uchaguzi Nigeria, hofu yatanda!

Mahakama Kuamua Matokeo Ya Uchaguzi Nigeria, Hofu Yatanda! Mahakama kuamua matokeo ya uchaguzi Nigeria, hofu yatanda!

Wed, 6 Sep 2023 Chanzo: Bbc

Mahakama ya Abuja ambayo imekuwa ikipima uhalali wa uchaguzi wa rais wa Februari itatoa uamuzi wake. Inaweza kusababisha ushindi wa Bola Tinubu kubatilishwa.

Uamuzi wa kumpata mshindi wa uchaguzi wa urais wa Februari 25 nchini Nigeria unaendelea mjini Abuja.

Mahakama itaamua kuhusu maombi yaliyopelekwa mbele yake na wagombea wa upinzani wa People’s Democratic Party, Labour Party na Allied People’s Movement wanaotaka kubatilisha tangazo la Rais Bola Tinubu kuwa mshindi wa uchaguzi huo.

Matarajio ya uamuzi huo yamezua hali ya wasiwasi kote nchini kufuatia uchaguzi huo wenye mgawanyiko mkubwa.

Katika mji mkuu, idadi kubwa ya askari na maafisa wa polisi wameweka vizuizi vya barabarani katika maeneo ya kimkakati katikati mwa jiji.

Inaonekana kuna hofu kwamba hukumu inaweza kusababisha maandamano, kulingana na nani atapoteza leo.

Kesi hiyo inaoneshwa moja kwa moja kwenye televisheni ili kuwa wazi kabisa, mahakama ilisema - ingawa ilikataa kuruhusu matangazo ya moja kwa moja wakati wa kusikilizwa kwa mawakili.

Chanzo: Bbc