Mon, 25 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mahakama ya Kikatiba nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imebatilisha ushindi wa Wabunge 40 kwasababu ya shutuma za makosa mbali mbali katika ushindi uliotangazwa miezi miwili iliyopita.
Wabunge hao 40 wanaishutumu Mahakama Kuu ya kikatiba kwa kushindwa kuwatendea haki wengi wao wakishutumiwa kuhusika katika wizi wa kura na viashiria vya kuvuruga uchaguzi uliopita.
Hata hivyo, wamefahamisha kuwa wanakwenda kukataa rufaa kuhusiana na hatua hiyo iliyochukuliwa na Mahakama hii ikiwa si mara ya kwanza kwa hatua kama hiyo kuchukuliwa nchini DRC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live