Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mahabusu achomoka mikononi mwa polisi wakiwa mahakamani

0fgjhs4834180qhm2 Mahabusu achomoka mikononi mwa polisi wakiwa mahakamani

Tue, 25 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Polisi mjini Mombasa wanamsaka mshukiwa wa wizi wa kimabavu ambaye alipokonyoka mikononi mwa polisi wakati wakiwa mahakamani Jumatatu, Mei 24.

Mshukiwa huyo, Ngala Hassan ambaye anakabiliwa na tuhuma za wizi wa kimabavu eneo la Likoni alihepa baada ya kuruka ukuta wa mahakama ya Mombasa baada ya dhamana yake kukataliwa.

Hassan ambaye alikuwa ameachiliwa kwa dhamana hapo awali alikamatwa tena na kuwasilishwa mahakamani Jumatatu kwa kudinda kuhudhuria vikao vya mahakama, suala lililomchochea jaji kufutilia mbali dhamana yake.

Muda mfupi baada ya makahama kutoa uamuzi wake kuhusu dhamana yake, mshukiwa aliomba kwenda msalani.

Alisindikizwa msalani na alipofika mlangoni, alifunguliwa pingu ili apate kujisaidia.

Punde si punde, mahabusu huyo aliripotiwa kuchomoka msalani mbio kabla ya kumgonga polisi aliyekuwa akimlinda mlangoni na kumuangusha chini.

Juhudi za afisa huyo kupiga kamsa na hata kumfyatulia risasi ziliambulia patupu kwani mshukiwa tayari alikuwa ametoweka.

Mshukiwa huyo aliingia mfichoni baada ya kuhepa kwa kuruka ua la mahakama hiyo.

Takriban miezi kadhaa iliyopita, mfungwa mmoja katika eneo la Turbo, kaunti ya Kakamega alimuosha polisi na mkojo ndoo nzima kabla ya kuhepa kizuizini.

Polisi walisema mshukiwa Benjamin Maloba ambaye alikuwa akifanya usafi katita seli aliomba asindikizwe msalani ili kumwaga uchafu ambao alikuwa ameubeba katika ndoo.

"Iliripotiwa na Josephat Thuranira ambaye alikuwa akimlinda mfungwa aliyekuwa akisafisha afisi za kituo, alikuwa akimsindikiza mfungwa huyo kwa jina Benjamin Maloba kwenda kumwaga chooni ndoo iliyojaa mkojo kutoka kwenye seli ya kiume," ripoti ya polisi ilisema.

"Mfungwa huyo alimuosha polisi huyo na mkojo usoni kabla ya kushika njia na kutokomea katika msitu wa karibu."

Kisanga hicho kilijiri takriban mwezi mmoja baada ya mshukiwa mwingine kuhepa kizuzini huko Tana River baada ya kumpaka polisi kinyesi.

Ripoti ya polisi ilionyesha kwamba mfungwa huyo Abdul Awadh mwenye umri wa miaka 19 na ambaye alikuwa anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Bura aliomba ruhusa ya kuelekea msalani.

Hata hivyo, polisi walifanikiwa kumnasa Awadh baada ya oparesheni kali ya kumsaka kuanzishwa.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke