Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazetini Oktoba 27: Waiguru asema wakazi ndio walimshinikiza asukume wilibaro

3a4c5aded3bbe6af Magazetini Oktoba 27: Waiguru asema wakazi ndio walimshinikiza asukume wilibaro

Wed, 27 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

1. The Standard Gazeti hili limeangazia hatua ya Gavana wa Kirinyaga, Anne Waiguru kuhama kambi ya Rais Uhuru Kenyatta na kuyoyomea katika chama cha William Ruto cha United Democratic Alliance (UDA).

Waiguru ambaye alijibandua kutoka chombo cha Uhuru siku ya bathdei yake ya 60, alisema katika mkutano wa faragha na Ruto kuwa ilikuwa vigumu kufanya mikutano ya kisiasa Kirinyaga sababu ya kushirikiana na Jubilee.

Diwani ambaye jina lake lilibanwa na gazeti hili alifichua kuwa wakati wa mkutano huo wa faragha, gavana huyo alisema kuwa wakazi wa Kirinyaga ndio walimshinikiza asukume wilibaro iwapo anataka kuwahutubia akiongezea kuwa baadhi ya jamaa zake tayari walikuwa ndani ya UDA.

Akitaja Sikukuu ya Mashujaa, Waiguru aliibika gavana wa kwanza Mlima Kenya kutangaza hadharani kumuunga mkono Ruto akisema ishara zote zilikuwa wazi kulingana na namna alimkaribisha naibu rais kuwahutubia wananchi.

2. Daily Nation Kulingana na gazeti hili, Spika wa Bunge la Kitaifa Justin Muturi amekubali kuwania urais mwaka 2022 akitumia tikiti ya Chama cha Democratic.

Read also

Gavana Lee Kinyanjui Amsonyea Waiguru kwa Kuingia UDA: "Harusi Inaanza Januari"

Muturi, siku ya Jumanne, Oktoba 26, alithibitisha kwamba atapeperusha bendera ya chama hico.

Chama hicho kilibuniwa na rais mstaafu Mwai Kibaki.

Mwezi uliopita, chama hicho kilimwalika Spika huyo kuwania urais kupitia kwa tikiti chake.

Muturi, akisifu chama hicho, alisema kitawaunganisha wakazi wa eneo la Mlima Kenya na bado alikuwa hajachagua chama cha kutumia kuwania urais hadi Jumanne.

3. Taifa Leo Katika gazeti hili , kesi kuhusu ubadhirifu wa KSh 231 bilioni za Huduma ya Vijana kwa Taifa(NYS), huenda itatupwa nje kwa kujikokota mahakamani.

Kesi hiyo ambayo inamshirikisha aliyekuwa Katibu Mkuu wa Masuala ya Vijana Lilian Mbogo-Omollo na mshtakiwa mwenzake imekuwa kortini tangu Mei 2018.

Kulingana na sheria za Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi, kesi za ufisadi zinatakiwa kuchukuwa muda wa miezi 24 pekee kukamilika.

Kesi hiyo ya NYS haijasikizwa tena tangu mwaka 2019 na mnamo Mei 2020, iliahirishwa sababu ya janga la COVID-19 ambalo lilitatiza vikao vya mahakama.



Read also

Purity Ngirici Amkaribisha Waiguru Chamani UDA, Aapa Atanyakua Tikiti ya Ugavana

4. The StarKatika The Star, kinara wa Amani National Congress, Musalia Mudavadi ameshikilia kuwa hatafuta azma yake ya kuwania urais 2022.

Mudavadi ambaye alisema tayari ameanza kuweka mipango madhubuti, alisema bado atakuwa kwenye debe mwaka 2022.

Alisema Wakenya hawatakani kubebwa na madai ya fahali wawili pekee ndio watanamenyana kwenye kivumbi hicho.

Mudavadi aliongezea kuwa tayari ameandaa manifesto yake ambayo ataizindua hivi karibuni.

5. People DailyKulingana na People Daily, Seneti limezuiwa kuwahoji magavana kuhusu ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu pesa za kukarabati barabara na pesa zilizotolewa na Benki ya Dunia kwa maendeleo ya miji ya Kenya.

Jaji Hedwig Ong'udi alitoa amri hiyo ya muda hadi kesi iliyowasilishwa na baraza la magavana itakaposikizwa na kuamuliwa.

Kesi hiyo itaisikizwa Oktoba 28.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke