Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazetini Ijumaa Aprili 23: Murathe matatani kisa zabuni ya KSh 4b kutoka Kemsa

C3629433144cb80c Magazetini Ijumaa Aprili 23: Murathe matatani kisa zabuni ya KSh 4b kutoka Kemsa

Fri, 23 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Ijumaa, Aprili 23, magazeti mangi ya humu nchini yanamzungumzia makamu mwenyekiti wa Chama cha Jubilee David Murathe ambaye alidaiwa kushawishi kampuni aliyokuwa akihusishwa nayo kushinda zabuni ya KSh 4 bilioni kuuzia Shirika la Kununua Bidhaa za Matibabu (Kemsa) vifaa vya kujikinga dhidi ya maambukizi (PPE).

Magazeti hayo pia yanaripoti kuhusu hila zinazozunguka ripoti ya Mchakato wa Maridhiano (BBI), baada ya kubainika kuwa kulikuwa na nakala tofauti tofauti za Mswada wa Marekebisho ya Katiba, na hali hiyo inafanya mchakato mzima kuwa katika hali ya atiati.

1. People Daily Gazeti hili linatanguliza kwa kueleza jinsi makamu mwenyekiti wa Chama cha Jubilee David Murathe alivyosababisa kampuni aliyokuwa akihusishwa nayo kushinda zabuni ya KSh 4 bilioni katika Shirika la Usambazaji wa Vifaa vya Tiba (Kemsa).

Hii ilifichuliwa kupitia nyaraka zilizowasilishwa na Kamati ya Bunge ya Uwekezaji wa Umma.

Mbunge wa Wajir Mashariki Rashid Amin alimshtumu Murathe kwa kile alichokitaja kuwa kutumia ukaribu wake na serikali kushawishi mikataba.

Lakini katika hati ya kiapo, Murathe alikanusha kuwa mkurugenzi, mbia, au mmiliki mwenye faida wa Kilig Limited ambayo alipewa zabuni ya kuuzia Kemsa Vifaa vya Kujinginga Dhidi ya Maambukizi (PPEs).

2. The StarJarida hili la kila siku liliripoti kuhusuana na jinsi United Democratic Alliance (UDA), chama kipya cha kisiasa kinachohusishwa na Naibu Rais William Ruto, kunavyojiandaa ili kukatiza talaka yake na chama tawala.

Katika hali ya kushangaza, UDA ambacho kimekuwa kikiweka wagombea kukabiliana na Jubilee katika chaguzi ndogo za hivi karibuni kimeandikia Msajili wa Vyama vya Siasa kikisema michakato ya usuluhishi inayofaa inapaswa kufanywa ili kutatuza mgogoro baina yao.

Lakini Jubilee kupitia kwa katibu mkuu wake Raphael Tuju kimeshikilia kuwa muungano na Party of Development and Reforms (PDR), sasa UDA, hauwezekani.

Washirika wa karibu wa Ruto katika siku za nyuma wamekuwa wakikiamia Juilee kuthubutu kukiondoa UDA kutoka kwa makubaliano yao ya muungano, wakisema wako tayari "kupambana hadi mwisho".

3. Daily NationKando na ripoti kuhusu zabuni ya KSh 4 bilioni kutoka Kemsa iliyopewa kampuni inayohusiana na Murathe kwenye ukurasa wake wa mbele, gazeti hilo linaripoti kwamba wawakilishi wadi wameomba Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kufafanua zaidi juu ya jinsi matoleo tofauti ya Mswada wa BBI yalivyopelekwa katika kaunti kujadiliwa.

Hii ni baada ya ripoti kuibuka kuwa angalau mabunge 34 ya kaunti huenda yalipewa matoleo tofauti ya Katiba ya Kenya (Mswada wa Marekebisho wa 2020).

Katibu wa Sekretarieti ya BBI Paul Mwangi alisema hakuna wanachoweza kuelezea kwani waraka huo ulitumwa moja kwa moja hadi IEBC.

Lakini kulingana na gazeti hilo, IEBC imejitenga na suala hilo, ikisema watetezi wa Mswada ndio walioleta nakala zote za waraka huo.

4. The StandardMbali na kuripoti kuhusu utata kuhusu BBI, gazeti hili pia limezungumzia kuhusu mkutano wa Alhamisi, Aprili 22, kati ya mwenyekiti wa KANU Gideon Moi na kaimu balozi wa Merika nchini Kenya Eric Kneedler.

Kulingana na gazeti hilo, viongozi hao walikutana jijini Nairobi ambapo walijadili masuala anuwai yanayolenga kuimarisha uhusiano wa pamoja kati ya Kenya na Merekani.

Masuala yaliyojadiliwa ni pamoja na biashara, usalama, mabadiliko ya hali ya hewa, na janga la COVID-19.

"Nchi hizi mbili zina changamoto za kawaida na tumepata njia kadhaa mpya za kufanya kazi pamoja ili kuboresha uhusiano wa kibiashara, uhusiano wa watu," alisema Kneedler.

5. Taifa LeoGazeti hili limeangazia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu Kihara Kariuki kuhusiana na mahakama kutengua maamuzi mengi ya Rais Uhuru Kenyatta.

Siku ya Jumanne, Aprili 20, Mahakama ya Juu ilitoa uamuzi wa kihistoria kuhusiana na nafasi za makatibu wa Baraza la Mawaziri na Maafisa Wakuu wa Utawala (CAS).

Korti ilitangaza katika uamuzi wake na kusema nyadhifa za CAS kuanzia mwaka wa 2018 ni kinyume cha katiba, hatua ambayo imepata pigo kubwa kwa utawala wa Jubilee.

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali pia ilishutumiwa kwa kuunda nafasi za Utendaji ambazo ni haramu na ambazo zimekuwa zikifanywa kwa lengo la kumpendeza Uhuru.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690. Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke