Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti ya Jumatatu, Novemba 8: Ruto amjibu Kalonzo ataka watangetange pamoja

03ef4c8992a1f3e6 Magazeti ya Jumatatu, Novemba 8: Ruto amjibu Kalonzo ataka watangetange pamoja

Mon, 8 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Novemba 8, yameripotia pakubwa kuhusu siasa za urithi za mwaka 2022, pande zote zikipanga mikakati ya kushinda kiti cha urais.

Magazeti haya pia yameguzia mwaliko wa Naibu Rais William Ruto ambaye amemkaribisha Kalonzo Musyoka katika kambi ya Tangatanga siku chache baada ya kiongozi huyo wa Wiper kuonyesha dalili ya kutaka kufanya kazi naye.

1. The Standard Ruto amewakaribisha wawaniaji wengine wa urais wanaotaka kufanya kazi naye.

Naibu wa rais alisema yuko tayari kubuni seriklai ijato na viongozi wenine ambao wanaoamini katika ndoto yake.

Matamshi ya Ruto yanaonekana kumlenga kinara wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka ambaye Jumamosi, Novemba 6, alisema kuwa yuko tayari kujiunga na kambi ya Ruto.

Makamu wa rais wa zamani alisema japo Ruto hajamfikia kwa mazungumzo ya kubuni muungano, yuko tayari kuzungumza naye (Ruto) sababu ni lazima Wakenya wafanye mashauriano.

Katika jibu lake, Ruto alisema yuko tayari kujiunga na wanaounga mkono lengo lake.

"Tuko wazi na tunawakaribisha viongozi wote ambao wako tayari kuungana nasi katika kuinua nchi hii chini ya mtindo wetu wa bottom up. Tumejiandaa kwa wale wanaotaka kufanya kazi nasi," naibu rais alisema Jumapili, Novemba 7, akiwahutubia waumini wa kanisa la AIPCA St Joseph eneo la Kikopey, Nakuru.

2. Daily Nation Katika gazeti hili, kiongozi wa ODM Raila Odinga ana KSh 150 bilioni ambazo anatumainia kutumia kuwaokoa Wakenya maskini iwapo atashinda uchaguzi mwakani.

Raila atakuwa anapiga kampeni yake chini ya msingi wa kuwasaidia Wakenya maskini.

Daily Nation linaripoti kuwa mpango huo utawagharimu walipa ushuru KSh 12 bilioni kila mwezi.

Mradi huo utakuwa unapiga jeki ahadi yake ya KSh 6,000 kila mwezi za kuwasaidia vijana wasiokuwa na ajira.

Akiulizwa namna atafadhili mradi huo, Raila alisema ataziba nyufa zote za ufisadi.

3. People Daily Raila atatangaza rasmi azma yake ya kuwania urais mwaka 2022 mnamo Disema 9, People Dailylimeripoti.

Licha ya dalili zote kuwa atajaribu kuwania kiti hicho kwa mara ya tano, Raila amekuwa akinyamazia azma hiyo.

Sasa anasema atatoa tangazo rasmi na kutoa mwelekeo kwa wafuasi wake.

Amekuwa akipiga ziara nchini kuhamasisha vuguvugu lake la Azimio la Umoja ambalo litakuwa uti wa mgongo wa kaeni zake za 2022.

"Nimekuwa nikizunguka kote nchini nikiunganisha watu. Nimesalia na eneo la Ukambani, South Rift na Nairobi. Nitatangaza iwapo nitashiriki kwenye kura Desemba 9 Nairobi," Raila alisema Jumapili, Novemba. 8, huko Makongeni, Nairobi, ambako alikuwa amehudhuria ibada ya kanisa iliyoongozwa na Legio Maria.

4. Taifa Leo Gazeti hili linaripoti kuwa Ruto amewakaribisha vinara wa One Kenya Alliance (OKA) kujiunga naye katika siasa za 2022.

Ruto amekuwa akivumisha kampeni yake ya urais 2022 kupitia mfumo wa uchumi wa bottom-up ambao alisema utawainu Wakenya wa kawaida.

Naibu Rais sasa amesem ayuko tayari kujiuna na viongozi wengine hususan baada ya Kalonzo kusema atajiunga na Ruto iwapo atamuomba.

"Tunawakaribisha kwa timu yetu wale walio na ajenda sawa na yetu. Ikiwa wako tayari, tunawaalika kwenye ndege. Nchi yetu ina changamoto nyingi ambazo zinaweza tu kutatuliwa na viongozi wote wanaoungana pamoja," alisema Ruto.

5. The Star Ruto anatazamiwa kufanya ziara ya siku tatu katika eneo la Nyanza wiki hii.Atazuru Kisumu, Migori na Homa Bay.

Ziaa yake katika kaunti ya Migori inakujia baada ya wiki mbili.

Ruto ataandamana na wanasiasa kutoka kaunti hizo tatu.

Kati ya kaunti hizo tatu Migori ndio humpokea Ruto kwa mbwembwe hususan kutokana na uhusiano wake na Gavana Okoth Obado.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke