Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti ya Jumanne, Novemba 30: Rais Uhuru kuhutubia taifa mara ya mwisho leo

D981bfeb98ffe509 Magazeti ya Jumanne, Novemba 30: Rais Uhuru kuhutubia taifa mara ya mwisho leo

Tue, 30 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumanne, Novemba 30, yanaendelea kuangazia siasa za urithi za mwaka 2022 yakimupa kipaumbele kinara wa Orange Democratic Movement (ODM) Raila Odinga anapotafuta mgombea mwenza wa mbio za kuingia Ikulu.

Magazeti haya pia yamegusia hotuba ya mwisho ya Rais Uhuru Kenyatta kwa taifa leo mchana akitazamia kuzungumzia uchumi na janga la COVID-19.

1. Daily NationKulingana na gazeti hili, mchakato wa Raila kumsaka mgombea mwenza wa chaguzi za 2022 unaripotiwa kuwalenga wagombeaji watatu.

Wapanga mikakati kutoka kambi ya Uhuru na Raila wamekubaliana kwa pamoja kwamba mgombea mwenza atateuliwa kutoka Mlima Kenya, lakini hawatambui ni nani atateuliwa.

Duru zinaarifu kuwa wagombeaji wa zamani wa urais Peter Kenneth na Martha Karua na Gavana wa Nakuru, Lee Kinyanjui ndio wanapigiwa upatu kwa wadhifa huo.

Hata hivyo, wachanganuzi wa siasa, bado wanajaribu kuwapiga msasa ni nani kati ya watatu hao ndiye bora zaidi kuwa naibu wa Raila.

2. Taifa LeoUfufuzi wa uchumi ulioathiriwa na janga la COVID-19, hatari ya virusi vipya, usalama wa kitaifa na hatua dhidi ya tabia nchi ni baadhi ya masuala yatakayoangazaiwa leo katika hotuba ya Uhuru.

Katika hotuba yake ya kila mwaka ambayo itakuwa ya mwisho, Uhuru ataripotia kuafikia malengo ya kitaifa, ugatuzi na uongozi bora.

Pia huenda akagusia malumbano kati ya Idara ya Mahakama na Serikali Kuu.

Kiongozi wa taifa pia anatazamia kuwashinikiza wabunge kutunga sheria zitakazosaidia serikali kutekeleza ajenda ya mabilioni ya pesa inayolenga sekta tofauti.

3. The StandardKatika gazeti hili, mkuu wa Idara ya Upelelezi George Kinoti amepata pigo kubwa baada ya Mahakama Kuu kukataa kubatilisha amri ya kumkamata na kufungwa jela.

Kinoti anatuhumiwa kudharau mahakama alipoamriwa kumrejeshea mwanabiashara Jimmy Wanjigi bunduki zake.

Kinoti alishikilia kuwa ni heri afungwe jela lakini hawezi kutoa bunduki hizo baada ya Jaji Anthony Mrima kumhukumu kifungo cha miezi minne jela kwa kupuuza mahakama.

Kinoti alisema Bodi ya kutoa leseni za bunduki ilifuta leseni ya Wanjigi hivyo hastahili kumiliki bunduki.

4. People DailyVinara wa One Kenya Alliance (OKA) wameitisha mkutano wa dharura leo asubuhi kujadili uvumi unaoendelea kuenea miongoni mwao na wandani wao kuhusu kuwaunga mkono wagombeaji wa vyama vingine.

Ajenda kuu katika mkutano huo ni madai kuwa vinara wa muungano huo na wandani wao wanafanya mkutano kisiri na Naibu Rais William Ruto na Raila.

Madai kuwa baadhi ya vinara wa OKA wamekuwa wakifanya mikutano na washindani wao yanachangia uhasama na mpasuko katika muungano huo wa kisiasa.

OKA umekuwa na matumaini ya kumteua mgombeaji wake wa urais katika chaguzi za 2022.

5. The StarRuto amesema haitaji kutawazwa na deep state kushinda Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Alisema atatafuta ungwaji mkono kutoka kwa mwananchi wa kawaida.

Naibu wa Rais alidai kuwa washindani wake wanasubiri kutawazwa na serikali.

Alizungumza Jumatatu nyumbani kwake Karen wakati alikutana na wanachama 3,000 wa kundi la Wamama na Hustler, linalounga mkono azma yake ya urais.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke