Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti ya Alhamisi, Agosti 5: Aliyeuawa na mpenziwe azikwa kando ya mumewe

99fb06ae6f7634a9 Magazeti ya Alhamisi, Agosti 5: Aliyeuawa na mpenziwe azikwa kando ya mumewe

Thu, 5 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Alhamisi, Agosti 5, yameripotia pakubwa kuhusu kutibuka kwa ziara ya Naibu Rais William Ruto nchini Uganda baada ya kuzuiwa kuondoka Uwanja wa Ndege wa Wilson.

Magazeti haya pia yameguzia taarifa ya jamaa kwa jina Jonathan Mukundi ambaye alimpiga risasi mke wake Philomena Njeri, kabla ya kujigeuzia bunduki na kujiua katika kaunti ya Kiambu.

1. Daily Nation Gazeti hili linaripoti kuwa Joyce Nyambura, ambaye anadaiwa kuawa na mpenziwe mtaani Kahawa West, alizikwa kando ya marehemu mume wake katika kijiji cha Gatitu, kaunti ya Kiambu.

Mama huyo mwenye umri wa miaka 34, anaripotiwa kuawa Jumatatu, Agosti 2, na jamaa huyo ambaye ameingia mafichoni baada ya wawili hao kutofautiana kuhusu mpango wake wa kusafiri Qatar kufanya kazi.

Marehemu, mama wa watoto watatu, alizikwa Jumatano, Julai 4, kando na kaburi la mume wake katika hafla iliyohudhuriwa na familia yake na marafiki.

Waliozungumza katika hafla hiyo walimuomba Mungu awalipizie kisasi.

Read also

Mpeni William Ruto Amani Baada ya Kumpokonya Majukumu Yake, Oscar Sudi

Kifo chake kimewaacha wanawe watatu mayatima na hivyo waombolezaji walichangisha pesa za kuwasaidia kurudi shuleni.

Watoto wake walimtaja kama mama bora ambaye hawezi kutwaliwa.

2. The Standard Gazeti hili linaripoti kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Usalama Karanja Kibicho alisema Ruto alikosa skakabathi muhimu kwa ziara yake ya Uganda.

Kibicho alisema hiyo ndio kiini pekee ya Ruto kuzuiwa kusafiri.

Hata hivyo, hakubainisha ni stakabithi zipi naibu rais alikosa kuwa nazo.

Katika mahojiano, Ruto alidai kuwa alizuiwa kusafiri kwa sababu ya kukosa kibali ya ziara yake.

Alifichua kuwa hii ilikuwa mara ya kwanza kuagizwa kutoa kibali katika miaka tisa kama Naibu Rais.

3. The Star Wazazi wawili wanataka Bunge la Kitaifa kufanyia uchunguzi matokeo ya mtihani wa KCPE 2020 wakitaja ubaguzi uliowakumba watahiniwa wa shule za kibinafsi.

Mary Njoki na Isaac Njoroge walisema matokeo ya wanao si sawa.

Wawili hao walitaja uwezekano wa kubatilishwa kwa matokeo hayo ili kuzipa shule za umma kipaumbele dhidi ya shule za kibinafsi.



Read also

Joyce Wanjiru: Picha za Mrembo Aliyeuawa na Mpenziwe Akijiandaa Kusafiri Qatar

Walizua malalamishi kuwa kusahishwa na mpangilio wa kutoa mtihani wa KCPE hauna uwazi na hivyo kumuweka Waziri wa Elimu George Magoha taabani.

Wanataka Kamati ya Bunge kuhusu Elimu kuchunguza madai ya ufisadi wakati wa zoezi la usahishaji.

4. People Daily Mwanabiashara Jimi Wanjigi aliibua wasiwasi katika Chama cha Orange Democratic Movement (ODM) baada ya kufanya misururu ya mikutano na baadhi ya wagombeaji ambao wanapanga kuwapokonya nyadhifa wandani wa kiongozi wa chama hicho Raila Odinga.

Wanjigi sasa anatuhumiwa kupanga njama ya kuwatumia wandani wa muda mrefi wa Raila katika chaguzi za 2022.

Mwanabiashara huyo ambaye alikuwa mfadhili mkuu wa kampeni za kiongozi huyo wa Upinzani katika Uchaguzi Mkuu wa 2017, alitangaza kuwania urais kupitia tikiti ya ODM.

5. Taifa Leo Gazeti hili linaripoti kuwa madiwani wa kaunti ya Kisumu wameshutumiwa vikali kwa kufanya ziara ya wiki moja ya mafunzo nchini Tanzania.

Madiwani hao wanaripotiwa kuzuru taifa hilo jirani kujifunza kuhusu uchukuzi ziwani na jinsi wakazi wa Kisumu wanaweza kufaidi kutokana na rasilimali zilizoko Ziwa Victoria.



Wakazi walisema inasikitisha kuwa ziara hiyo ilijiri wakati kaunti ya Kisumu inaathirika na makali ya janga la COVID-19 na ukosefu wa fedha.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke