Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti: Viongozi wa kidini wapanga kumfanyia Uhuru na Ruto handisheki

Efb24e5277055174 Magazeti: Viongozi wa kidini wapanga kumfanyia Uhuru na Ruto handisheki

Mon, 6 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Septemba 5, yameripotia fujo iliyoshudiwa kati ya mirengo ya Jubilee mjini Nyeri, Naibu Rais William Ruto alipokuwa akihudhuria ibada.

Magazeti haya pia yameguzia uhasama wa Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake ambao umetatiza mikutano ya baraza la mawaziri kwa zaidi ya miezi sita sasa.

1. Daily NationGazeti hili linaripotia namna ziara ya Ruto eneo la Kieni lilikumbwa na fujo baada ya kundi la vijana kujaribu kumzuia na kurushia mawe msafara wake.

Awali, ripoti zilidai kuwa makanisa makubwa katika eneo bunge hilo yalimkataa naibu rais ambaye alikuwa anatarajiwa kuhudhuria ibada katika Kanisa la Full-Gospel, Mbiriri.

Kanisa hilo la mabati halingeweza kupokea kikosi kizima cha Ruto na hivyo kuamua kuandaa ibada ya Jumapili katika uwanja wa Mbiriri.

Hata hivyo, maafisa wa polisi waliokuwepo walikataa kuruhusu hema kuwekwa katika uwanja huo wakidai kutopewa kibali.

Wandani wa Ruto walimlaumu Mbunge wa Kieni, Kanini Kega kwa fujo hiyo ambaye ni mshirika wa karibu wa rais.

Kega anashtumiwa kuwakodisha wahuni kutibua ziara ya Ruto eneo hilo.

Akihutubia wakazi ambao walikuwa wamekusanyika kando ya barabara, Ruto alisema bado ataendelea na safari yake ya kuelekea Ikulu na hakuna kitakchomzuia.

Alidai kuwa serikali imeanza kutatiza azma yake lakini alishikilia kuwa hatishwi.

2. The StandardKulingana na The Standard, baraza la mawaziri la Uhuru halijakutana kwa zaidi ya miezi sita ikishirikishwa na uhasama na naibu wake.

Wanaojiunga na Uhuru ni sehemu ya wale ambao wanampiga Ruto.

Hivi majuzi Waziri wa Usalama wa ndani Fred Matiang'i alimshtumu Ruto kwa kugeuza serikali.

Matiang'i alimtaka Ruto ajiuzulu na kuwa upinzani kwa kukiuka serikali na juhudi zake za kutoka ndani.

Wengine ambao wako kwenye rekodi ya kumshutumu Ruto ni waziri wa Mawasiliano Joe Mucheru, ambaye alimkashifu Ruto kwa kuwatumia vijana kwa faida zake binafsi.

Kutokana na hayo, mabadiliko yanarajiwa kufanyia baraza la mawaziri.

3. People DailyKutokana na mpasuko kati ya Uhuru na Ruto, viongozi wa kidini wamejitolea kuwapatanisha wawili hao.



Viongozi sita wakuu wa kidini wanasemekana kushinikiza kuwepo kwa mkutano kati ya wawili hao wiki hii.

Wandani wa wawili ndio wanalaumiwa kwa mvutano kati yao.

Sita hao Anthony Muheria wa Kanisa la Katoliki Dayosisi ya Nyeri, Silas Yego aliyekuwa mkuu wa AIC,Jackson Ole Sapit wa ACK, Philip Anyolo wa Kanisa Katoliki Dayosisi ya Kisumu, Robert Lang'at wa Knisa la African Spell na David Oginde aliyekuwa mkuu wa CITAM, wanatazamia kuwapatanisha wawili hao ambao wamekuwa wakipigana vita baridi kwa miaka mitatu.

Ruto amekuwa akilaumu handisheki ya Uhuru na kiongozi wa ODM, Raila Odinga kwa masaibu hayo.

4. Taifa Leo Kulingana na gazeti hili, Ruto alikataliwa na makanisa matatu eneo la Kieni kuhudhuria ibada Jumapili, Septemba 5.

Alitumia muda wake katika Kanisa la Full-Gospel Mbiriri ambalo halingeweza kuwabeba zaidi ya watu 100.

Maafisa wa polisi waliokuwepo walikataa kuruhusu hema kuwekwa katika uwanja huo wakidai kutopewa kibali.



5. The Star The Star limeripotia tanda belua linalowakumba wandani wa Ruto eneo la Mlima Kenya.

Wandani wa Ruto wamewashtumu wenzao kwa kukataa kujiunga na UDA kikamilifu.

Mbunge wa Gatundu Kusini, Moses Kuria na Mwangi Kiunjuri, wanadaiwa kuwa washirika wa Ruto lakini wamedinda kuingia UDA.

Kuria alishikilia kuwa eneo hilo linahitaji chama ambacho kitapigania haki ya wakazi.

Anaongoza Chama Cha Kazi (CCK) ambacho kimeshirikiana na cha Martha Karua, Narc Kenya na cha Kiunjuri, The Sevice Party (TSP).

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke