Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Septemba 8: Ruto aumwa na kichwa kumtafuta mgombea mwenza

2b3af1e5fc820902 Magazeti Septemba 8: Ruto aumwa na kichwa kumtafuta mgombea mwenza

Wed, 8 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatano Septemba 8 yanaendelea kuangazi kuhusu vigogo wa kisiasa na mikakati yao kuhusu uchaguzi mkuu ujao wa 2022.

Aidha kuna taarifa pia kuhusu majangili ambao wanawahangaisha wakazi wa Laikipia huku mshirikishi wa bonde la Ufa George Natembeya akionekana kuingiwa na maji kuwahusu.

The Star

Gazeti la Star lina habari kuhusu uhalifu ambao unaendelea Laikipia huku wezi wa mifugo waliojihami vikali wakizua hofu.

Tayari hata maafisa wa polisi wameingiwa na maji huku mshirikishi wa Bonde la Ufa George Natembeya akisema majangili hao wamejihami kuliko hata maafisa wa polisi.

Natembeya alisema wanatumia bunduki za hali ya juu kuwaliko maafisa wa polisi na hivyo kuwatisha pakubwa.

Inaarifiwa kuna mpango wa kuwatuma maafisa wa KDF ili kusaidia kukabiliana na kundi hilo hatari.

Standard

Gazeti la Standard limeangazia taarifa kuhusu mzozo kati ya naibu rais William Ruto na Rais Uhuru Kenyatta kwenye serikali ya Jubilee.

Rais amekuwa akijaribu kumtimua DP kutoka serikalini akiwatumia wandani wake lakini Ruto amekuwa imara kutokana na kulindwa na katiba.

Read also

Magazeti Jumatatu, Septemba 6: Ruto Azuiwa Kuingia Kanisani

Mwandishi anasema iwapo wandani wa Rais wataamua kumuondoa DP, basi itabidi watafute wabunge wengi ili kuunga mkono mswada wa kumuondoa serikalini.

Daily Nation

Nation inaangalia kitendawili cha naibu rais katika kumtafuta mgombea mwenza kwenye uchaguzi wa 2022.

Baadhi ya wale ambao analenga ni Gavana Anne Waiguru, Mwangi Wairia, Kiriatu Murungi, aliyekuwa waziri Mwangi Kiunjuri, Seneta Kithure Kindiki na Spika Justin Muturi.

Wengine ni mwanasiasa wa Gatanga Peter Kenneth na Waziri Peter Munya ambao wandani wa DP wanawapiga msasa.

Taifa Leo

Taifa leo imeangazia taarifa kuhusu Jubilee kuwa na mpango wa kumtimua naibu rais William Ruto kutoka chama cha Jubilee.

Katibu wa Jubilee Raphael Tuju alisema chama kimeandikia kamati ya kitaifa NMC wakitaka Ruto atimuliwe kwa kuendeleza ajenda za chama kingine.

Tuju alimshambulia DP akisema wamekuwa akijihusisha na UDA licha ya kuwa naibu kiongozi wa chama cha Jubilee.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke