Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti: Rais asema 2022 mchague mzee, wachaneni na kijana pumzi itamuishia

Bd6f658de4c4a5bf Magazeti: Rais asema 2022 mchague mzee, wachaneni na kijana pumzi itamuishia

Thu, 2 Dec 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Alhamisi Disemba 2 yameangazia taarifa kuhusu uchaguzi mkuu ujao baada ya Rais Uhuru Kenyatta kusema 'mzee' ndiye atawika 2022.

Akiongea mjini Nakuru Jumatano Disemba 1 Rais alionekana kumlima naibu wake William Ruto akisema alianza siasa za urais mapema na hivi karibuni ataishiwa na pumzi.

Star

Jarida hili linasema Rais Uhuru Jumatano Disemba 1 aliashiria kinara wa ODM Raila Odinga ndiye chaguo lake katika kurithi Ikulu 2022.

Rais alitumia mafumbo kuwaonya Wakenya dhidi ya kumchagua naibu wake William Ruto akisema amekosa subira ya kuchukua uongozi.

Alisema DP amekuwa akienda kwa kasi sana bila kujua kuwa siasa za kuchukua uongozi na kama mbio za nyika ambazo huanza polepole.

Aidha alikashifu siasa za ubaguzi kwa mirengo ya umri akisema wazee ndio wenye maarifa katika kile kilionekana kama kutetea Raila Odinga ambaye ana miaka 76.

Daily Nation

Nation nayo imeangazia taarifa za kutimuliwa kwa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko kutoka afisini.

Mahakama ya Rufaa iliarifiwa kuwa kuondolewa kwa Sonko hakukufuata sheria kwani hakukabidhiwa ushahidi wa makosa aliyokuwa ameadhibiwa kuyahusu.

Mawakili wa Sonko walisema MCAs hawakufuata utaratibu unaohitaji kabla ya gavana kutimuliwa.

Aidha walisema mahakama ya Juu ilidinda kufuatilia jinsi ambavyo sheria ilikosa kufuatwa na bunge hilo wakati wa kumfukuza Sonko.

Standard

Gazeti hili limeripoti kuhusu sintofahamu iliyopo kuhusu watakaposomea wanafunzi wa gredi 6, 7 na 8 ambao watakuwa wakijulikana kama Junior Secondary.

Wakurugenzi wa masomo katika kaunti wanasema walipokea ujumbe wahakikishe kuna madarasa katika shule za msingi yatakayotumika kama Junior Secondary.

Hata hivyo, katibu katika wizara ya Elimu amepinga hilo akisema Junior Secondary haiwezi kuwa katika shule za msingi

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke