Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Oktoba 18: Raila aanza kufuta nyayo za Ruto na mfumo mpya

6f796453c680f82d Magazeti Jumatatu, Oktoba 18: Raila aanza kufuta nyayo za Ruto na mfumo mpya

Mon, 18 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Oktoba 18, yameipa uzito siasa za urithi za mwaka 2022 huku upande wa upinzani ukibuni mikakati kabambe ya kutwaa ushindi.

Magazeti haya pia yameripotia kuhusu ukaguzi wa mali ya maafisa wa serikali huku Seneti ikipanga kujadili mswada huo.

1. Daily NationKulingana na gazeti hili, Rais Uhuru Kenyatta na mwenzake wa handisheki Raila Odinga wako kwenye mpango wa kubuni mrengo wa kisiasa utakaotumika katika uchaguzi wa urais wa 2022.

Wawili hao watatumia wazo la mrengo wa Rainbow ambao rais mstaafu Mwai Kibaki alitumia kutwaa mamlaka 2002.

Mrengo huo unapania kuzima usawishi wa Naibu Rais Willam Ruto, ambaye anaonekana kuwa tishiokwenye mbio hizo za kuwania urais.

Chama tawala cha Jubilee na upinzani ODM vinafanya mazungumzo ya kuhakikisha wanashinda kiti cha urais.

Vyama hivyo katika kampeni zao vinalenga mambo matatu yaliyotumiwa na Narc mwaka 2002, ambayo wanatumainia yatakuwa ya maana katika uchaguzi ujao.

2. The StandardKatika gazeti hili, Ruto alianz akupia kampeni baada ya serikali ya Jubilee kumtena.

Katika kampeni zake za miaka miwili, Ruto ameweza kuteka mateka maeneo ambayo yana ukwasi wa kura hususan Mlima Kenya.

Kampeni zake zimekuwa zikimuweka kifuambele dhidi ya mahasidi wake wanaomezea mate kiti cha urais.

Hata hivyo bahati ya Ruto inaonekana kudidimia baada ya hasidi wake mkubwa Raila, kuanzisha kampeni ya 'Azimio La Umoja' ambayo imekuwa ikiwavizia wapiga kura.

Kampeni za Raila zimeonekana kuzima juhudi za Ruto.

Kutokana na hayo, The Standard inashangaa iwapo Ruto atakuwa akiongoza mbio ama kuwa mdhibiti wa mbio.

Lakini Ruto anaonekana kutokata tamaa huku akivamia ngome za Raila hivi majuzi akizuru eneo la Pwani.

3. People Daily Mswada mpya umewasilishwa katika Bunge la Seneti ambao utawalazimu maafisa wa serikali na jamaa zao mali zao kukaguliwa.

Mswada huo kwa sasa upo kwenye hatua ya pili na unatarajiwa kujadiliwa Jumanne, Oktoba 19.

Iwapo mswada huo utapitishwa, maafisa wote wa serikali akiwemo rais na naibu wake ni lazima mali zao zitakaguliwa na kuwekwa wazi.

4. Taifa Leo Taifa Leo linaripoti kuwa vijana wanawakaidi wazee katika chaguo lao kuelekea chaguzi za 2022.

Wazee katika maeneo tofauti wamekuwa wakitoa kauli zao kuhusu ni nani wanapendelea kuwa rais.

Kwa mfano katika baraza la wazee la Muyoot miongo mwa Kalenjin, wamegawanyika katika kumchagua Ruto.

Katika eneo la kati mwa Kenya, mgawanyiko huo umekuwa ukishuhudiwa huku wakiwateua wagombeaji wao.

Baadhi yao wamemteua Spika Justin Muturi, wengine wakimuunga mkono Ruto wengine wakimuegemea kinara wa ODM Raila Odinga.

5. The Star Raila atarejea katika eneo la Mlima Kenya kutafuta ungwaji mkono.

Kinara wa ODM atatua katika kaunti za Tharaka Nithi, Meru na Embu.

Raila atapokelewa na magavana watatu Muthomi Njuki (Tharaka Nithi), Kiraitu Murungi (Meru) na Martin Wambora(Embu) .

Waziri wa Kilimo Peter Munya pia anatazamiwa kuandamana na Raila wakati wa ziara hiyo.

Hata hivyo kuna uwezekano Munya atasusia mkutano huo sababu ya uhasam wake na Kiraitu.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke