Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Novemba 22: Ruto apungua umaarufu kisiasa Raila akiimarika

2c3c58fb2ef40cea Magazeti Jumatatu, Novemba 22: Ruto apungua umaarufu kisiasa Raila akiimarika

Mon, 22 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Novemba 22, yameripotia pakubwa siasa za 2022 huku kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka akiitisha mkutano wa kujadili nafasi yake ya kuwania urais.

Magazeti haya pia yameguzia masharti mapya ya Wizara ya Afya ya kuwafungia nje wale ambao hawajachanjwa chanjo ya COVID-19 kupata huduma za serikali.

1. The Star Katika The Star, kiongozi wa Wiper, Kalonzo Musyoka anatazamiwa kufanya mkutano na wajumbe wa chama hicho kuhusu azma yake ya kugombea urais 2022.

Makamu huyo wa zamani wa rais amekuwa njia panda iwapo atawania kiti hicho na wakati mmoa kudokeza kuwa anataka kuungana na Naibu Rais William Ruto.

Mkutano wa wajumbe wa chama hicho utatoa mwelekeo kuhusu hatma yake kisiasa.

Mwaka ujao Kalonzo atakuwa anajaribu mara ya pili kuwania urais iwapo atagombea.

Katika chaguzi mbili zilizopita amekuwa mgombea mwenza wa Raila.

2. The Standard Muungano wa One Kenya Alliance (OKA) umeshikilia kuwa utaendelea na mpango wake wa kumteua mgombeaji wao wa urais mwakani.

Muungano huo unawaleta pamoja Kalonzo wa Wiper, kinara wa KANU Gideon Moi, Musalia Mudavadi wa ANC na mwenzake wa Ford Kenya, Moses Wetangula.

Mnamo Jumapili, Novemba 21, wanne hao walifanya mikutano kadhaa ya hadhara mjini Naivasha ambapo walipigia debe muungano wao licha ya mvutano baina yao.

Kalonzo alifutilia mbali ripoti za vyombo vya habari kuwa OKA unakaribia kuvunjika akifichua kwamba wanatumainia kuwaalika wanachama wengine.

Kumekuwa na ripoti ya malumbano OKA huku vyama tanzu vikilaumiana kwa usaliti.

Cleophas Malala alikuwa amekashifu KANU kwa kulemaza muungano huo.

3. Daily Nation Gazeti hili linaripotia vita kati ya aliyekuwa Jaji Mkuu David Maraga na wakili Ahmednassir Abdullahi almaarufu Grand Mullah.

Maraga amefungua kesi dhidi ya Grand Mullah kuhusiana na madai ya kumharibia jina.

Wakili huyo alidai kuwa Maraga alipata cheo cha Jaji Mkuu kupitia kushawishi idara ya mahakama kila mara.

Kulingana na Grand Mullah, Maraga aliwahi kupokea hongo ya KSh 200 milioni kutoka kwa mmoja wa majaji wa Mahakama ya Upeo.

4. People Daily

People Daily inaripoti kuwa Wakenya ambao hawajachanjwa hawatapokea huduma za serikali kuanzia Disemba 21, 2021.

Kulingana na Waziri wa Afya Mutahi Kagwe, yeyote anayetafuta huduma ya serikali ni lazima awe na cheti cha kupokea chanjo ya COVID-19.

Kagwe alisema kuwa wizara yake ikishirikiana na serikali za kaunti na washikadau wengine itafanya zoezi ya kuchanaj halaiki kwa siku kumi kuanzia Novemba 26.

“Hakuna aliyesema chanjo ni lazima, lakini ukitaka huduma za serikali lazima uchanjwe dhidi ya virusi hivyo,” alisema Kagwe.

Huduma hizo za serikali ni kama vile KRA, Elimu, Uhamiaji, Hospitali, NTSA, na Bandari.

5. Taifa Leo Gazeti hili limeripotia kupungua kwa makali ya Ruto kuelekea uchaguzi mkuu wa 2022.

Utafiti uliofanywa na Tifa ulionyesha kuwa umaarufu wa Naib Rais unaendelea kudidimia licha ya kuongoza katika mbio za kuwania urais.

Kura ya maoni ilionyesha kuwa Ruto ana umaarfu wa 38%akifuatwa na Raila, ambaye ana asilimia 23%.

Hata hivyo, utafiti huo ulibaini kwamba umaarufu wa Ruto unapungua huku wa Raila ukiendelea kuhimarika.

Katika eneo la Mlima Kenya, Raila ana ungwaji mkono mkubwa akiungwa mkono na magavana wote kando na Gavana wa Kirinyaga, Anne Waiguru, ambaye alihama Jubilee na kujiunga na UDA.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke