Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Novemba 15: Mahasla wapigania pesa za Ruto

19907a3fd5f03048 Magazeti Jumatatu, Novemba 15: Mahasla wapigania pesa za Ruto

Mon, 15 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Novemba 15, yameangazia siasa za 2022 ambazo zinaendelea kupamba moto kila kuchao huku Naibu Rais William Ruto akichomoa pesa zaidi kunoa makali yake nan kuwanasa wapiga kura.

Magazeti haya pia yamegusia mpasuko katika muungano wa One Kenya Alliance (OKA), ambapo vinara wake wameshindwa kumteua mpeperushaji wa bendera ya urais.

1. Daily NationGazeti hili linaripoti kuwa washawishi wakubwa katika kampeni za Ruto wamekuwa wakificha pesa ambazo amekuwa akitoa kama mchango wa kuwafaidi wahudumu bodaboda na wanabiashara wengine wadogo.

Wale ambao wanatakiwa kupokea pesa hizo wamelalamikia kupigwa chenga na waandalizi wa kampeni za Naibu Rais.

Katika visa kadhaa, makundi yamekuwa yakitofatiana na kulaumiana kuhusu pesa walizopewa kugawana.

Wiki jana sehemu ya vijana katika eneo la Mwingi, kaunti ya Kitui waliandamana kushtumu kutoweka kwa KSh 3 milioni zinazoripotiwa zilitolewa na Ruto kama mchango kwa vyama vya bodaboda na wafanyabiashara wengine wadogo.

Wiki hiyo hiyo, vita vilizuka wakati wa ziara ya Ruto katika eneo la Kondele, Kisumu polisi wakidai vurugu hizo zilitokana na kugawana pesa.

Wiki hii Ruto atakuwa katika kaunti za Tharaka Nithi na Meru.

Daily Nation linaripoti kuwa tayari vyama vya bodaboda vimeanza kutofautiana kuhusu watakavyogawana pesa kabla ya ziara ya Ruto katika kaunti hizo mbili.

2. The Standard Kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi amekosoa ahadi za Ruto na waziri mkuu wa zamani Raila Odinga wakijiandaa kwa mbio za kuwania urais 2022.

Akizungumza Jumapili, Novemba 14, katika ibada ya kanisa kwenye Barabara ya Ngong, Mudavadi alisema ahadi za wawili hao ni feki akiongeza kuwa wanazitumia kuwanasa Wakenya.

Alikosoa ahadi ya Raila ya kutoa KSh 6,000 kila mwezi kwa familia maskini akisema hali ya sasa ya uchumi haiwezi kufadhili mradi huo.

Kuhusu ahadi ya Ruto ya KSh 150 bilioni kwa vijana na akina mama, Mudavadi alisema taifa limefilisika na itakuwa vigumu kwa mpango huo kutekelezwa.

Alisema Wakenya wataongezewa ushuru kufadhili mipango hiyo iwapo itatekelezwa na Ruto ama Raila.

3. Taifa Leo

Gazeti hili pia limeangazia michango ya Ruto ambayo imekuwa chanzo cha vurugu.

Katika kila mkutano wake wa hadhara, Ruto amekuwa akitoa pesa za kuwasaidia wafanyabiashara wadogo na makundi ya kujiwezesha.

Makundi hayo sasa yanataka Ruto awe akiwapa pesa moja kwa moja wakishtumu washirika wake kwa kuwapiga chenga kila pesa zinapotolewa.

Wiki jana sehemu ya vijana katika eneo la Mwingi, kaunti ya Kitui waliandamana kushtumu kutoweka kwa KSh 3 milioni.

4. The Star Gazeti hili limeguzia mpasuko katika muungano wa One Kenya Alliance (OKA), ambapo vinara wake wameshindwa kumteua mpeperushaji wa bendera ya urais.

Muungano huo umewaleta pamoja kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi, kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka, Moses Wetangula wa Ford Kenya na Gideon Moi wa KANU.

Katika muungano huo, Seneta Moi amekuwa akidhihirisha kumpendelea Raila, akidokezea mipango ya kufanya kazi pamoja naye.

Kwa upande wake Mudavadi, amekuwa akishikilia kwamba hatakuwa mgombea mwenza wa mgombeaji yeyote wa urais wandani wake wakitishia kujiondoa iwapo hatatajwa kuwania urais.

Hivi majuzi, Kalonzo alionyesha tamaa yake ya kutaka kuungana na Ruto akisema yuko tayari kufanya mazungumzo naye.

Wetangula bado yuko kimya kuhusu hatma yake baada ya kutumikia kaunti ya Bungoma kwa mihula miwili kama Seneta.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke