Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Novemba 1: OKA wamkaidi Uhuru, wamkataa Raila

E4c84217bdef3454 Magazeti Jumatatu, Novemba 1: OKA wamkaidi Uhuru, wamkataa Raila

Mon, 1 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Novemba 1, yameipa uzito siasa za urithi za 2022 ambapo muungano wa One Kenya Alliance (OKA) umeapa kushiriki.

Vinara wa OKA wamekataa kile walitaja kulazimishwa na Rais Uhuru Kenyatta kumuunga mkono mgombeaji mwingine wa urais ambaye jina lake halikutajwa.

1. The Star Muungano wa One Kenya Alliance (OKA) umemkashifu Uhuru kwa kuwa kizingiti katika mpango wa kumteua mgombeaji wao wa urais katika uchaguzi wa mwakani.

Siku ya wikendi, vinara wa muungano huo wanasemakana kufanya nkutano na Rais katika Ikulu.

OKA uliwaleta pamoja kiongozi wa KANU Gideon Moi, Musalia Mudavadi wa ANC, Kalonzo Musyioka wa chama cha Wiper Party na kinara wa Ford Kenya, Moses Wetangula.

Mnamo Ijumaa, Octoba 29, wanne hao walizindua kampeni zao Kakamega kabla ya kuitwa ikulu.

Wanne hao saa wanamlaumu Uhuru kwa kukatiza kampeni zao wakiapa hawatakubali presha yake ya kuwataka wamuunge mkono mgombejai tofauti.

"Kwa nini OKA inapokuwa na hafla, simu hutoka Ikulu? Sasa inadhihirika kuwa tukiwa na hafla Ikulu itakuwa ikipiga simu. Huo unaweza kuwanufaisha watu wawili pekee, kinara wa ODM Raila Odinga au DP William. Ruto,” alisema Kibisu Kabatesi, msaidizi wa Mudavadi.

2. Daily Nation Katika gazeti hili, kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka huenda atakuwa mfalme wa siasa katika kivumbi cha uchaguzi wa urais mwakani.

Makamu wa zamani wa rais anamezewa mate na Ruto na Raila, ambao wote wamejitosa kwenye kinyanganyiro cha kumrithi Uhuru.

Kando na hayo, Kalonzo amekuwa akishikilia kuwa hatakuwa mgombea mwenza wa yeyote akisisitiza kuwa atawania urais.

Licha ya msimamo wake mkali, wataalam wanasema kuwa huenda mwishowe Kalonzo atakubali kumuunga mkono Raila.

Wakati huo huo, wanachama wakuu wa wa Wiper wamekuwa wamuumiza kuendelea na azma yake ya kuwania urais.

3. The Standard The Standard limeangaza kibarua kigumu cha Uhuru kuwashawishi vinara wa OKA kujiunga na Raila kwa uchaguzi mkuu wa 2022.

Kuna uwezekano kuwa huenda Raila atamteua mgombea mwenza kutoka Mlima Kenya na kuwaacha vinara wa OKA kwa mataa.

Awali, kaka hao wa handisheki walikuwa wanaegemea mswada wa Mpango wa Maridhiano ambao ungelipanua serikali kuu ili kuwajumuisha wapinzani.

4. Taifa Leo Licha ya kufanya mkutano na Uhuru wikendi, vinara wa OKA wameshikilia msimamo wao kuwa hawatamuunga mkono mgombaji mwingine wa urais.

Akihutubia wakazi wa Thika Jumapili, Octoba 31, kiongozi wa ANC Musalia Mudavai alisema Wakenya ndio wataamua akiongezea kuwa muungano huo hautakubali presha ya Ikulu ya Nairobi.

Rais anamtafutia Raila majemedari.

5. People DailyHuku chaguzi za 2022 zikikaribia, wanasiasa wanatumia kila namna kuwafikia wapiga kura.

Vyama vimewekeza mitandaoni ambayo ndio bora zaidi katika karne ya sasa.

Wagombeaji sasa wanatafuta huduma za mabloga ambao watawasaidia kusukuma ajenda yao kupitia mitandaao ya kijamii.

Propaganda ndio imekuwa njia bora ya wanasiasa kutumia kuwakabili mahasidi wao.

Mabloga ndio wanajulikana kuwa vifaa katika kueneza propaganda na hivyo kuwasaidia wagombejai kupata nafasi ya kukabiliana na mahasidi wao.

Kwa sasa mabloga ambao huduma zao zinapiganiwa ni ikiwemo Dennis Itumbi, Robert Alai na Cyprian Nyakundi.

Itumbi na Alai tayari wamekita kambi kwa Ruto na Raila mtawalia.

Kwa upande wake Nyakundi, hajakuwa akionyesha msiamamo wake wala kumuegemea yeyote.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke